Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (mwenye kofia) akipata maelezo ya hali
ya sekta ya mifugo na Uvuvi kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Kanali Denis
Mwila (mwenye suti nyeusi) alipotembelea kituo cha mpakani cha Mutukula leo.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (mwenye kofia) akipokea maelezo ya
changamoto za ukaguzi mazao ya mifugo na Uvuvi kutoka kwa Afisa Uhamiaji
Konstabo, Rahabu Joel alipotembelea kituo cha mpakani cha Mutukula leo.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (mwenye kofia) akiangalia mabondo ya
samaki aina ya Sangara yaliyokamatwa katika kituo cha mpaka cha Mutukula
mkoani Kagera. Kulia ni kaimu Mkurugenzi wa Idara ya maendeleo ya Uvuvi
Mwanaidi Mlolwa katikati Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Missenyi Limbe
Maurice. Kilo120 zilikamatwa katika kituo hicho.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akifungua mlango wa gari lililokamatwa
na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ngara likiwa limepakia samaki kilo
2,000 aina ya Sangara na kilo 530 wa aina ya Sato zenye thamani ya shillingi
20,850,000/= kwenye mpaka wa Mlusagamba wilayani Ngara tarehe 03/12/2017.
Na John Mapepele
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Joelson Mpina ya Halmashauri ya Wilaya ya
Ngara kuhakikisha inafufua mara moja mnada wa Mlusagamba ifikapo mwezi
Februari mwaka huu ili kudhibiti zaidi ya milioni mia moja zinazopotea kwa
wafanyabiashara wanaokwepa kulipa kodi ya Serikali ya kusafirisha mifugo nje ya
nchi kwa kupita njia za panya.
Waziri Mpina aliyasema haya leo alipokutana na uongozi wa Halmashauri hiyo
pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ngara katika kituo cha
mpaka cha Rusumo baina ya Tanzania na Rwanda kukagua shughuli mbalimbali za
sekta za Mifugo na Uvuvi baada ya kutokea katika kituo cha Mutukula mkoani
Kagera ambapo pia alifanya ukaguzi kama huo na kukamata kilo 120 za mabondo
ya samaki aina ya Sangara yaliyokuwa yakitokea nchi jirani ya Uganda bila kufuata
utaratibu.
“Mimi kama Waziri mwenye dhamana ya sekta ya mifugo na uvuvi naelekeza
kwamba ifikapo Februari mwaka huu nataka miundo mbinu yote iwe
imeboreshwa na mnada wa Mlusagambo uwe unafanya kazi katika kiwango cha
mnada wa upili na mimi mwenyewe nitahakikisha ninakuja kuuzindua”lisisitiza
Mpina
BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI
BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...