Na Agness Francis, Globu ya jamii

KAMPUNI ya simu za mkononi Airtel Tanzania, imeendelea kutoa zawadi kwa wateja wake kupitia promosheni ya SMATIKA yatosha na Intanenti Bando inayoendelea kufanyika nchini.

Ambapo wateja wa Airtel hujishindia GB na zawadi zingine ikiwa ni simu za mkononi aina ya Smartphone na Modern ya Maajabu. Pia leo kampuni hiyo imemkabidhi mshindi wa simu aina ya Smartphone Mussa Ngai ambaye ni mkazi wa Vingunguti jijini Dar es Salaam. 

Akizungumza leo jijini, Meneja Uhusiano Airtel Jackson Mmbando baada ya makabidhiano hayo akiwa kwenye duka la Airtel money Ukonga Mzambarauni Dar es salaam kuwa sasa wamefikia droo ya 10 kufanyika katika promosheni hiyo ambayo bado inaendelea kwa siku 30 zaidi. 

"Tumetimiza wateja 21,000 waliojishindia GB za bure na 30 waliojishindia simu na Modern ya maajabu kwa wateja wetu endeleeni kununua bando ili muweze kujishindia zawadi mbalimbali kutoka kwetu,"amesema Mmbando. 

Aidha Msimamizi wa duka la Airtel money Ukonga Mzambarauni Dorice Opiyo amewakaribisha wateja ambao ni wakazi wa maeneo hayo kupata huduma za kurejesha laini na kujipatia salio kwa wale wanatoa huduma za mawaka

Mshindi wa simu aina ya Smartphone, Mussa Ngai mkazi ambaye ni mkazi wa Vingunguti jijini Dar es Salaam, akizungumzia kushinda promosheni hiyo amesema amefurahi kushinda kwani hakutegemea na alikuwa akinunua bando na kujiunga mpaka siku alipopigiwa simu kutoka Airtel ya kuambiwa ameshinda simu aina ya Smartphone.
 Mshindi wa Smartphone Mussa Ngai akikabidhiwa zawadi leo na  Dorice Opiyo Msimamizi wa Brunch ya Airtel Money Ya Ukonga Mzambarauni Jijini  Dar es salaam.
Mshindi wa simu ya Smartphone   Mussa Ngai  akikagua simu yake mara baada ya zoezi la makabidhiano kumalizika leo katika  tawi la Airtel Money Ukonga Mzambarauni Jijini  Dar es Salaam.
 Mshindi wa simu ya Smartphone  Mussa Ngai akipiga picha na wasimamizi wa Brunch ya Airtel money Ukonga Mzambarauni Jijini Dar es Salaam mara baada ga kukagua zawadi yake aliyoshinda kupitia promosheni ya SMATIKA na yatosha Intanenti bando.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...