Na Agness Francis, Globu ya jamii
KAMPUNI
ya simu za mkononi Airtel Tanzania, imeendelea kutoa zawadi kwa wateja
wake kupitia promosheni ya SMATIKA yatosha na Intanenti Bando
inayoendelea kufanyika nchini.
Ambapo wateja wa Airtel hujishindia GB na zawadi zingine ikiwa ni simu za mkononi aina ya Smartphone na Modern ya Maajabu. Pia
leo kampuni hiyo imemkabidhi mshindi wa simu aina ya Smartphone Mussa
Ngai ambaye ni mkazi wa Vingunguti jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
leo jijini, Meneja Uhusiano Airtel Jackson Mmbando baada ya
makabidhiano hayo akiwa kwenye duka la Airtel money Ukonga Mzambarauni
Dar es salaam kuwa sasa wamefikia droo ya 10 kufanyika katika promosheni
hiyo ambayo bado inaendelea kwa siku 30 zaidi.
"Tumetimiza
wateja 21,000 waliojishindia GB za bure na 30 waliojishindia simu na
Modern ya maajabu kwa wateja wetu endeleeni kununua bando ili muweze
kujishindia zawadi mbalimbali kutoka kwetu,"amesema Mmbando.
Aidha
Msimamizi wa duka la Airtel money Ukonga Mzambarauni Dorice Opiyo
amewakaribisha wateja ambao ni wakazi wa maeneo hayo kupata huduma za
kurejesha laini na kujipatia salio kwa wale wanatoa huduma za mawaka
Mshindi
wa simu aina ya Smartphone, Mussa Ngai mkazi ambaye ni mkazi wa
Vingunguti jijini Dar es Salaam, akizungumzia kushinda promosheni hiyo
amesema amefurahi kushinda kwani hakutegemea na alikuwa akinunua bando
na kujiunga mpaka siku alipopigiwa simu kutoka Airtel ya kuambiwa
ameshinda simu aina ya Smartphone.
Mshindi
wa Smartphone Mussa Ngai akikabidhiwa zawadi leo na Dorice Opiyo
Msimamizi wa Brunch ya Airtel Money Ya Ukonga Mzambarauni Jijini Dar es
salaam.Mshindi wa simu ya Smartphone Mussa Ngai akikagua simu yake mara baada ya zoezi la makabidhiano kumalizika leo katika tawi la Airtel Money Ukonga Mzambarauni Jijini Dar es Salaam.
Mshindi wa simu ya Smartphone Mussa Ngai akipiga picha na wasimamizi wa Brunch ya Airtel money Ukonga Mzambarauni Jijini Dar es Salaam mara baada ga kukagua zawadi yake aliyoshinda kupitia promosheni ya SMATIKA na yatosha Intanenti bando.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...