Na Mwandishi Wetu, Arusha
Shirika la Kimataifa la Farm Africa limewataka wakulima wadogo wa mazao ya nafaka hapa nchini kutumia mifumo ya mitandao kupitia simu za mkononi kutangaza bei ya mazao ya nafaka na kupata taarifa za kilimo bora ili kuwasaidia kupata kipato chenye tija na kuondokana na hali duni katika familia zao.

Meneja Program ya FoodTrade wa Shirika hilo la Kimataifa la Farm Africa,Bi. Beatrice Muliahela alisema hayo jijini Arusha katika warsha ya siku moja kuwa wakulima wadogo wanahitajika kutumia mifumo ya mitandao kupitia simu katika kutangaza bei ya mazao yao na kupata taarifa za kilimo bora ili kuwasaidia kupata kipato chenye tija na kuondokana na hali duni katika familia zao.

Mradi huu ni wa miaka miwili na unafadhiliwa na Department for International Development (DFID) kupitia DAI kwa kuhusisha wadau wengine kama Taasisi ya Maendeleo Vijijini na Mijini (RUDI) na VECO kwa sasa Rikolto ambao umesaidia wakulima wadogo 70,000 nchini Tanzania na Uganda.

“Farm Africa inahitaji kuona wakulima wadogo nchini Tanzania wanatumia mifumo ya mitandao kupitia simu katika kutangaza bei ya mazao yao na kuuza kwa bei nzuri zaidi,” na hii tunahamasisha katika nchi zote kumi za Afrika Mashariki kutumia mifumo hii, aliongeza kusema,Bi. Muliahela.
 Mkurugenzi wa Msaidizi Kitengo cha Kuzuia Upotevu wa Mazao baada ya Mavuno Wizara ya Kilimo, Bi. Josephine Omolo kushoto akifuatilia mada katika warsha iliyokuwa ikizungumzia jinsi wakulima wanavyoweza kutumia mifumo ya mitandao kupitia simu za mkononi kutangaza bei ya mazao yao na kupata taarifa za kilimo bora na kipato chenye tija kuwawezesha kuondokana na hali duni katika familia zao, katikati ni Meneja Program ya FoodTrade wa Shirika la Kimataifa la Farm Africa,Bi. Beatrice Muliahela na kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Maendeleo Vijijini na Mijini (RUDI), Lameck Kikoka.
 Wadau wa Shirika la Kimataifa la Farm Africa wanaojihusisha na shughuli za kilimo wakifuatilia  mada katika warsha iliyokuwa ikizungumzia jinsi wakulima wanavyoweza kutumia mifumo ya mitandao kupitia simu za mkononi kutangaza bei ya mazao yao na kupata taarifa za kilimo bora na kupata kipato chenye tija kuwezesha kuondokana na hali duni katika familia zao. 
Meneja Program ya FoodTrade wa Shirika la Kimataifa la Farm Africa,Bi. Beatrice Muliahela akifafanua jambo katika warsha iliyokuwa ikizungumzia jinsi wakulima wanavyoweza kutumia mifumo ya mitandao kupitia simu za mkononi kutangaza bei ya mazao yao na kupata taarifa za kilimo bora kupata kipato chenye tija na kuondokana na hali duni katika familia zao, katikati ni Mkurugenzi wa Msaidizi Kitengo cha Kuzuia Upotevu wa Mazao baada ya Mavuno Wizara ya Kilimo, Bi. Josephine Omolo na kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Maendeleo Vijijini na Mijini (RUDI), Lameck Kikoka.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...