Na Leandra Gabriel, Globu ya Jamii 
IDARA ya Uhamiaji nchini imefanya operesheni katika Chuo Kikuu cha Kampala (Kampala International University - KIU) kilichopo Gongo la Mboto jijini Dar es salaam na kubaini uwepo wa wafanyakazi 37 wanaofanya kazi bila kuwa na kibali maalumu. 
Akizungumza na Michuzi Blog leo, Msemaji wa Idara hiyo, Bw. Ally Mtanda amesema kuwa baada ya kuwabaini wafanyakazi hao wanaofanya kazi kinyume na utaratibu idara hiyo imechukua maelezo kutoka kwa kila mfanyakazi na amesema baada ya uchunguzi kukamilika wengine wanaweza kwenda mahakamani na kwa wengine taratibu zingine za kiuhamiaji zitaendelea. 
Amesema kuwa kwa sasa wanachukua maelezo ili kuweza kujiridhisha juu ya kuwepo kwa na kafanya kazi nchini hapa. Bw. Mtanda amesema kuwa operesheni hiyo ni endelevu katika kubaini wahamiaji haramu na wanaoishi na kufanya kazi bila vibali nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...