Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akizungumza na wananchi wa Kahama
mkoani Shinyanga mara alipowasili katika wilaya hiyo kwa ziara ya kikazi ya
kuzungumza na maofisa na askari wa Jeshi hilo, IGP Sirro amewataka wananchi
hao kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi hilo pamoja na kuwafichua wahalifu
waliopo kwenye maeneo yao.
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia mkoa wa Shinyanga, wakiimarisha ulinzi
wakati Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, aliposimamisha msafara wake ili
kuzungumza na wananchi waliojitokeza barabarani katika mji wa Kahama mkoani
Shinyanga leo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga Simon Haule (aliyesimama) akitoa hotuba
mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, aliyewasili mkoani humo kwa
ziara ya kikazi yenye lengo la kuzungumza na Maofisa na askari wa Jeshi hilo na
kuwakumbusha kutimiza wajibu wao wa kutenda haki kwa wananchi
wanaowahudumia.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akiwa katika picha ya pamoja na askari wa
Kikosi cha Kutuliza Ghasia wa mkoa wa Shinyanga leo akiagananao mpakani mwa
mkoa huo na wilayani Mbogwe, Geita, IGP Sirro yupo mkoni humo kwa ziara ya
kikazi. Picha na Jeshi la Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...