Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani
Jafo, amemfagilia Mbunge wa Jimbo la Dodoma Anthony Mavunde kwa jitihada
zake za kuwaletea maendeleo kwa wananchi wake, huku akiuagiza Wakala wa
Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kuhakikisha katika bajeti yao ya
mwaka 2018/19 wanaingiza kwenye mpango ujenzi wa barabara ya lami
Chang’ombe hadi Chuo cha Mipango.
Jafo ameyasema hayo leo alipokuwa anazindua soko jipya la kisasa kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo kata Chang’ombe lililojengwa na Serikali kwa kusaidiana na wafanyabiashara na Mbunge Mavunde ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana.
Ujenzi wa soko hilo ulianza mwaka 2017 na kukamilika mapema mwaka huu na litakuwa na wafanyabiashara wa bidhaa mbalimbali takribani 342 na limegharimu kiasi cha Sh.Milioni 70.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Jafo amesema katika ziara zake za miradi ya maendeleo alizotembelea katika Manispaa ya Dodoma, Mbunge Mavunde ameonekana kushiriki katika kila sekta kwa kusaidiana na wananchi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk.Binilith Mahenge akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Jafo ameyasema hayo leo alipokuwa anazindua soko jipya la kisasa kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo kata Chang’ombe lililojengwa na Serikali kwa kusaidiana na wafanyabiashara na Mbunge Mavunde ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana.
Ujenzi wa soko hilo ulianza mwaka 2017 na kukamilika mapema mwaka huu na litakuwa na wafanyabiashara wa bidhaa mbalimbali takribani 342 na limegharimu kiasi cha Sh.Milioni 70.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Jafo amesema katika ziara zake za miradi ya maendeleo alizotembelea katika Manispaa ya Dodoma, Mbunge Mavunde ameonekana kushiriki katika kila sekta kwa kusaidiana na wananchi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk.Binilith Mahenge akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.

Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...