Na Said Mwishehe,Globu ya jamii 

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Willium Lukuvi amesema Dar es Salaam ndio inaongoza kwa migogoro mingi ya ardhi nchini.

Amesema ili kutafuta ufumbuzi wa migogoro ya ardhi ameanzisha kampeni inayofahamika kwa jina la Funguka na Waziri itakayotoa fursa kwa wananchi wenye migogoro kuifikisha wizarani na hatimaye kupata ufumbuzi.

Lukuvi amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua ambazo Wizara yao inachukua kutatua migogoro ya ardhi nchini.

Amesema Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi imedhamiria kushughulikia migogoro ya ardhi nchini na kwa mwaka huu yeye pamoja na Naiu Waziri wa wizara hiyo watazunguka maeneo mbalimbali nchini kuwasikiliza wananchi na kutatua migogoro iliyopo.

Kuhusu Dar es Salaam ,Lukuvi amesema ni Jiji ambalo linaongoza kwa migogoro ya ardhi nchini na kufafanua na wilaya inayoongoza ni Kinondoni hasa maeneo ya Tegeta na Mbezi.

"Siku chache zilizopita nimeshughulikia migogoro ya ardhi kwa Mkoa wa Dar es Salaam ambapo wananchi zaidi ya 400 nimewasikiliza na kupata ufumbuzi.Na leo hii nimerudi tena Dar es Salaam ambapo kwa leo tu wananchi 420 nitawasikiliza.

"Kwa Dar es Salaam migogoro inatokana na watu kudhulimiwa viwanja, mirathi na mingine watu kuvamia viwanja vya watu wengine na kisha kujenga.Pia ipo migogoro inayoshughulikiwa na Mahakama na iliyotolewa hukumu.

"Migogoro ambayo imetolewa hukumu wizara haina uwezo wa kuishughulikia ,hivyo tunashauri warudi tena mahakamani ili kupata haki. Hivyo tutaendelea kuishughulikia kadri ya uwezo wetu.Tutafanya hivyo kwa nchi nzima,"amesema Lukuvi.

Amefafanua leo, kesho na keshokutwa atakuwa Dar es Salaam na baada ya hapo atakwenda Kagera na kisha atarudi tena Kanda ya Pwani ambapo kuna Dar es Saalam na Pwani.

Akielezea zaidi jitihada zinazofanywa na wizara yake kutatua mgogoro ya ardhi, Lukuvi amesema wakati yeye na Naibu Waziri wakiendelea kushughulikia migogoro hiyo, pia watalaamu wa ngazi mbalimbali wizarani hapo nao wanaishughulikia.

"Ipo migogoro ambayo Waziri wa Ardhi anao uwezo wa kuitafutia ufumbuzi kutokana na mamlaka niliyonayo na ndio maana nimeamua kuwa na kampeni ya Funguka na Waziri ili kusikiliza wananchi.Hivyo kwenye kampeni kuna fomu maalumu ambazo zitajazwa na wananchi na tukifika kwenye mkoa husika watajulishwa ili tuwasikilize.

"Na kwa kuwa tutakuwa tunasikiliza wananchi maeneo ya wazi ,hivyo hata wale ambao watakuwa hawajaandikwa majina nao watasikilizwa,"amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...