Mbunge mstaafu wa Kilombero Mhe. Abdul Rajabu Mteketa amepelekwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaa kwa matibabu, baada ya Jumamosi Februari 11, 2018 kuomba msaada wa kupatiwa matibabu ya upasuaji wa magoti yake. 
Mbunge huyo aliyetumikia jimbo la Kilombero baada ya kushinda katika uchaguzi mkuu mwaka 2010, alitumia njia ya video mtandaoni kupeleka ujumbe kwa Rais na jana Jumapili gari la wagonjwa lilifika na kumchukua kumpeleka Muhimbili. Video ya kwanza inamuonesha Mhe. Mteketa akiomba msaada, unafuatia ukurasa wa Facebook wa mkewe unaomshukuru Rais kwa msaada huku ukisisitiza kuwa wao wasingeweza. Video ya pili inamuonesha mhusika akishukuru akiwa ndani ya gari la wagonjwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...