Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MGOMBEA ubunge jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Abdallah Mtulia ameendelea kuomba kura huku akiwaambi wananchi yeye hana tofauti na wao.

Pia shida za wananchi ni shida zake, matatizo yao ni matatizo yake pia na kuongeza yeye in mtoto wa kimaskini.tulia amesema hayo kwa nyakati tofauti kwenye mikutano yake ya kampeni kwenye uchaguzi huo wa jimbo hilo.Hata hivyo wakati Mtulia akiomba kura  kwa wananchi hao wa Kinondoni, mgombea ubunge wa Chadema Salum Mwalimu naye ameendelea kuomba kura.

Mwalimu amekuwa akitoa Sera mbalimbali zenye lengo kuleta maendeleo kwa wananchi wa jimbo na kwamba anaamini yeye ndio mgombea sahihi ,hivyo wamchague alete maendeleo.Wakati wagombea hao kila mmoja akiomba kura  za wananchi hao ,kwa Mtulia yeye ameendelea kusisitiza changamoto za jimbo hilo anazijua na anao uwezo wa kuzitatua.

"Niliguswa na matatizo yenu ya kubomolewa nyumba nikaenda Mahakamani kuzuia bomoabomoa nikafanikiwa."Nilipambana kuhakikisha watu waliobomolewa wanapata hifadhi Magomeni. Nimekuja CCM kuhakikisha hilo linatimia," amesema Mtulia. Ameongeza kuwa "Niliacha ubunge, mshahara, posho na kiinua mgongo changu kwa sababu nawajali wana Kinondoni. Ukiwa jiongozi wa upinzani hauwezi kufanya lolote.

"Maendeleo hayapatikani kwa kutukana, kukashifu, matusi. Maendeleo huja kwa ushirikiano na mahusiano mema," amesema.Amefafanua zaidi  ni kweli anampenda Rais,Dk.John Magufuli  na kuuliza ataachaje Rais ambaye anajenga reli ya kisasa, kununua ndege za kisasa, ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme. Rais mkweli na muwazi.
MGOMBEA ubunge jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) Abdallah Mtulia ameendelea kuomba kura huku akiwaambi wananchi yeye hana tofauti na wao.
Mbunge wa jimbo la Mtera,Livingstone Lusinde akimnadi Mgombea Ubunge jimbo la Kinondoni jana jioni katika viwanja vya Vegas,Makumbusho,Kinondoni jijini Dar. 
Baadhi ya Wananchi na wafuasi wa chama cha CCM wakiwa wamekusanyika kwenye kampeni katika viwanja vya Vegas,Makumbusho Kinondoni jijini Dar
Baashi ya Wananchi wakishangilia yaliyokuwa yakijiri kwenye kampeni hizo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...