Kampuni
inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali ya Tigo Tanzania, leo
imewazawadia washindi 36 wa promosheni ya Nyaka Nyaka Bonus simu aina ya
Tecno R6 zenye uwezo wa 4G.
Akitangaza
washindi hao wa kwanza 36 waliopatikana katika promosheni hiyo
inayoendelea kwa kipindi cha miezi mitatu, Meneja wa Mawasiliano wa
Tigo, Woinde Shisael alibainisha kuwa washindi 13 wanatoka Dar es
Salaam, na wengine ni wakaazi wa mikoa ya Morogoro, Pwani, Tanga,
Dodoma, Mtwara, Iringa, Mwanza na Arusha.
‘Ofa
hii kabambe ni sehemu ya ubunifu wa Tigo unaoendana na mahitaji ya
wateja na utakaowezesha kila mtu kufurahia huduma bora za mtandao wa
Tigo 4G wenye kasi zaidi na ulioenea zaidi nchini,’ alisema.
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kati) akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam alipotangaza washindi wa kwanza wa simu za Tecno R6 zenye uwezo wa 4G katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus. Tigo inatoa bonasi ya hadi GB1 ya intaneti kwa wateja wanaonunua bando za data kuanzia TSh 1,000 kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00# pamoja na fursa ya kushinda mojawapo ya simu za smartphone kila saa. Kushoto ni Mtaalam wa Bidhaa wa Tigo, Baraka Hamza.
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kulia) akimzawadia Saidi Abdallah Popote wa Tabata, Dar es Salaam simu aina ya Tecno R6 yenye uwezo wa 4G aliyoshinda katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus, huku akishuhudiwa na baadhi ya washindi wengine. Tigo inatoa bonasi ya hadi GB1 ya intaneti kwa wateja wanaonunua bando za data kuanzia TSh 1,000 kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00# pamoja na fursa ya kushinda mojawapo ya simu za smartphone kila saa.
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kati) akimzawadia Advera Revelian Kyaruzi wa Tegeta, Dar es Salaam simu aina ya Tecno R6 yenye uwezo wa 4G aliyoshinda katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus, huku akishuhudiwa na baadhi ya washindi wengine. Tigo inatoa bonasi ya hadi GB1 ya intaneti kwa wateja wanaonunua bando za data kuanzia TSh 1,000 kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00# pamoja na fursa ya kushinda mojawapo ya simu za smartphone kila saa.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...