Mkufunzi Mwandamizi wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi Tanzania, Balozi Peter Kallaghe(kushoto)
akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dkt Juma Malewa walipofanya ziara ya
mafunzo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza leo Februari 21, 2018(wa pili kulia) ni Kamishna wa Fedha
na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga.
Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dkt Juma Malewa akifanya mazungumzo mafupi na
Maafisa Wakufunzi(hawapo pichani)kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa cha Tanzania walipofanya ziara
ya mafunzo Makao Makuu ya Magereza leo Februari 21, 2018.
Maafisa Wakufunzi toka Chuo cha Ulinzi wa Taifa cha Tanzania wakisaini kitabu cha wageni
katika Ofisi ya Kamishna Jenerali wa Magereza kabla ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Jeshi la
Magereza Jijini Dar es Salaam(wa kwanza kushoto) ni Mkufunzi Mwandamizi wa Chuo cha Taifa cha
Ulinzi Tanzania, Balozi Peter Kallaghe.
Maafisa Washiriki kutoka Chuo cha Ulinzi wa Taifa cha Tanzania wakiangalia meza
iliyotengenezwa katika Kiwanda cha Uselemala cha Gereza Kuu Ukonga katika ziara yao ya mafunzo
katika Jeshi la Magereza.
Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga(kulia) akipokea zawadi kwa niaba
ya Kamishna Jenerali wa Magereza kutoka kwa Mkufunzi Mwandamizi wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi
Tanzania, Balozi Peter Kallaghe(kushoto).
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...