Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega amefanya ziara katika vijiji vya Kise, Kibululu na Kiparang'anda (B) Kata ya Kiparang'nda ili kujua changamoto mbalimbali zinazo wakabili wananchi na kuweza kuzishughulikia kupitia Halmashauri pamoja Ofisi yake.
Akizungumza na wananchi wa Vijiji hivyo amesema wakati wa sasa ni kufanya wa maendeleo ya kweli bila kuangalia itikadi za vyama.
Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kise Kata ya Kiparang'nda kuhusu changamoto mbalimbali zinazo wakabili wananchi hao.
Mkazi wa Mkuranga, Selemani Mpambika akiuliza swali kwa kwa Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi, ambae ni mbunge wa jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega wakati wa mkutano huo.
Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa jimbo la Mkuranga,, Abdallah Ulega (alieshika kikombe cha kahawa) akiwa sambamba na Wazee wa Mkuranga kwenye kijiwe cha kahawa akipata kikombe cha kahawa pamoja ambapo pia walibadilishana mawazo juu ya maendeleo ya wilaya yao.Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya jamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...