Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Kampuni ya King Lion imetoa msaada wa waendesha bodaboda waliopata ajali na wamelazwa katika Hospitali Taifa ya Muhimbili
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukakabidhi msaada huo Afisa Uhusiano na Masoko, Erasto Baragamba amesema kuwa kama kampuni inatambua umuhimu wa waendesha bodaboda hivyo wanatoa mchango ambao utasaidia kujisitili.
Msemaji wa waendesha bodaboda Wilaya ya Ilala, Abdallah Bakari amesema wanashukuru kinglion kwa msaada walioutoa.
Amesema waendesha bodaboda wazingatie sheria za usalama barabarani ili kuweza kuepukana na ajali zinazotokana na makosa ya kibinadamu.
Msemaji wa waendesha bodaboda wa Manispaa ya Ilala, Abdallah Bakari akizungumuza na waandishi habari kuhusiana msaada kwa waendesha bodaboda waliopata ajali na wamelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Msemaji wa waendesha bodaboda wa Manispaa ya Ilala, Abdallah Bakari akikabidhiwa msaada kutoka kwa Afisa Uhusiano na Masoko, Erasto Baramamba.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...