Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika Yang wamefanikiwa kutoka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya st Louis ya Visiwa vya Shelisheli katika mchezo uliochezwa leo Jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo wa kwanza katika hatua ya mtoano uliopigwa leo, ilichukua takribani dakika 67 kwa Yanga kuandika goli la kwanza na la ushindi kupitia kwa mchezaji wake Juma Mahadhi aliyeingia kuchukua nafasi ya ibrahim Ajib.

Yanga ilishindwa kutumia nafasi walizozipata katika kipindi cha kwanza ikiwemo penati aliyoipiga Obrey Chirwa na kuitoa nje.St Louis imepoteza mchezo wao wa kwanza lakini walionekana wakijilinda kwa mda wote.

Kocha msaidizi wa Yanga Shedrack Nsajigwa amesema kuwa wameona wapi walipokosea ila katika mchezo wa marudiano  utakaofanyika wiki mbili zijazo.

Yanga inahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili kuweza kufuzu hatua inayofuata ya Klabu Bingwa Afrika mechi itakayochezwa Februari 19 mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...