
MKUU wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga amewaongoza mamia ya wakazi wa viongozi wa Serikali na vyama vya siasa katika mazishi ya aliyekuwa mwanasiasa mkongwe nchini na Mwenyekiti msaafu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) mkoani Kigoma, Amani Kaburu.
Akizungumza katika msiba huo Brigedia Jenerali Maganga amesema Kaburu ni mwanasiasa aliyejikita kutetea haki za wananchi wa Kigoma na alikuwa wa kwanza kupigania maendeleo ya mkoa huo.Mwili wa Kaburu umepumzishwa jana kwenye nyumba yake ya milele.
Amesema Serikali na CCM itamkumbuka Kaburu kwa mchango mkubwa ambao ameufanya katika mkoa huo na amekuwa mfano wa kuigwa na wengine na licha kutangulia mbele ya haki ameacha alama.
"Marehemu Kaburu atakumbukwa kwa mchango wake na alipokuwa kiongozi wa vyama mbalimbali na hata katika Bunge la Afrika Mashariki.Hakika ameondoka lakini wana Kigoma tutamkumbuka daima na kwa wanasiasa wengi wanafahamu kuwa vijana wengi mkoani hapa wamejifunza siasa kutoka kwake,"amesema na kuongeza kifo cha Kaburu kimeacha pigo kubwa kwa Serikali, CCM, wananchi wa Kigoma na Watanzania kwa ujumla.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma Amandusi Nzamba amesema CCM imepata pigo kubwa kwa kumpoteza mwanasiasa huyo aliyekuwa mstari wa mbele kukisaidia chama hicho katika kufikia malengo yao.Wakati huohuo Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe amesema kama mtoto na mwanafunzi wa Kaburu pamoja na tofauti za kisiasa ndiye aliyekuwa mwalimu wao na aliwazibua masikio wanasiasa wengi wa Mkoa huo.

Baadhi ya Ndugu,Jamaa na Marafiki wakiwa kwenye mazishi ya Dkt Kaborou hapo jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...