Na Ismail Ngayonga.
WAWEKEZAJI
wa ndani na nje ya Tanzania wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuwekeza katika
miradi mikubwa ya ujenzi wa viwanda nchini kwani kwa sasa mradi wa kuzalisha
umeme wa Kinyerezi II unaotarajia kuzalisha megawati 240 umekamilika kwa
asilimia 90.
Hayo yamesemwa leo
Jijini Dar es Salaam na Meneja Miradi wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Mhandisi
Stephen Manda wakati wa ziara ya wajumbe wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB)
kukagua miradi mbalimbali inayosimamiwa na Bodi hiyo nchini.
Alisema kuwa hadi
sasa jumla ya mitambo minne kati ya mitambo nane ya mradi huo tayari imeanza
kufanya kazi, ambapo katika gridi ya taifa mitambo hiyo inapekeka megawati,
hivyo TANESCO imejipanga kuhakikisha kuwa ifikapo Septemba mwaka huu mitambo
yote ya mradi huo imeanza kufanya kazi ili kuyafikia mahitaji yote ya umeme
nchini.
Manda alisema
kukamilika kwa mradi wa umeme wa kinyerezi II ni moja ya mipango na mikakati ya
TANESCO ya kuongeza kiwango cha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini, hatua
inayolenga kujenga mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa sekta ya viwanda nchini.
Wajumbe wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi(ERB), wakiongozwa na Mwenyekiti wao Prof. Ninatubu Lema (mwenye miwani kushoto) wakifuatilia maelezo kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Mitambo ya Umeme wa Kinyerezi II,240 MW kutoka kwa Meneja Miradi wa Tanesco Mhandisi Steven Manda wakati wa ziara yao katika mradi huo leo jijini Dar es Salaam.
Meneja Miradi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Steven Manda(watatu kutoka kushoto) akiwapa maelezo kuhusu mradi wa ujenzi wa mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia wa Kinyerezi II,wajumbe wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi(ERB), wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Prof. Ninatubu Lema (mwenye miwani) wakati wa ziara yao katika mradi huo leo jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Kaimu Msajili wa Bodi ya hiyo Mhandisi Patrick Barozi. Mradi huu utazalisha umeme megawati 240 pindi utakapokamilika.
Mmoja wa Wahandisi wa Shirika la Usambazaji Umeme Tanzania (Tanesco) akionyesha namna wanavyosimamia uongozaji wa mitambo ya kuzalisha umeme katika mradi wa Kinyerezi II walipotembelewa na wajumbe wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi(ERB), wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Prof. Ninatubu Lema (mwenye miwani) leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Msajili wa Bodi ya hiyo Mhandisi Patrick Barozi. Mradi huu utazalisha umeme megawati 240 pindi utakapokamilika.
Picha ikionyesha
baadhi ya mitambo iliyopo katika mradi wa kuzalisha umeme kutumia gesi asilia
wa Kinyerezi II utakaozalisha jumla ya megawati 240 pindi utakapokamilika. (Picha na: Frank
Shija).
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...