KIKOSI cha Yanga kinashuka leo dimbani katika mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika wakiwa ugenini dhidi ya timu ya Welayta Dicha kutoka Ethiopia.

Yanga inayoshuka dimbani wakiwa na ushindi wa goli 2-0 walioupata wakiwa nyumbani katika mchezo uliochezwa April 7 mwaka huu.

Katika mchezo wa Kwanza Yanga waliweza kucheza bila nyota wake watatu wakitumikia adhabu ya kuwa kadi mbili za njano ambao wamejumuishwa kwenye kikosi cha kwanza cha leo.

Yanga wakiwa chini ya Kocha msaidizi Noel Mwandila na Shadrack Nsajigwa kitashuka dimban katika uwanja wa Hawasa kutafuta ushindi wa aina yoyote, sare au kutokufungwa goli zaidi ya moja.

Matokeo hayo yanambeba Yanga na wataweza kuingia katika hatua ya Makundi ya kombe la Shirikisho ambapo wataweza kujinyakulia kitita cha mamilioni.

Youthe Rostand
Hassan Ramadhan 
Haji Mwinyi
Abdallah Shaibu 'Ninja'
Kelvin Yondani

Pappy Tshitshimbi
Thabani Kamusoko
Raphael Daud
Pius Buswita

Obrey Chirwa
Yusuf Mhilu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...