KAMPUNI
ya mafuta ya Puma Energy Tanzania imejivunia ufanisi wa huduma ya
mafuta iliyotoa kwa ndege kubwa aina ya Airbus 380 inayomilikiwa na
Shirika la Ndege la Emirates iliyotua kwa dharura Uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Kwa mujibu wa Meneja Idara ya Mafuta ya Ndege wa kampuni hiyo, Raymond Tungaraza alisema hatua hiyo ni sehemu ya uthibitisho kuwa Tanzania kupitia kampuni ya Puma Energy ina uwezo wa kutosha kutoa huduma ya nishati hiyo hata kwa ndege kubwa zaidi duniani.
“Uwezo wa kutoa huduma ya nishati ya mafuta kwa ndege kubwa kama hizi tena kwa ufanisi ni moja ya kivutio muhimu kwa mashirika mengine makubwa kuweza kuleta ndege zao hapa nchini hasa kipindi hiki ambapo Serikali imejipanga kuleta mageuzi katika sekta ya anga hivyo Puma Energy Tanzania tunajivunia kuwa sehemu ya kuwezesha mageuzi hayo,’’ alisema.
Akizungumzia zoezi hilo lililofanyika mapema siku ya Jumatano kabla ndege hiyo haijaondoka hapa nchini kuelekea Mauritius, Meneja wa Kituo cha Mafuta cha kampuni hiyo kilichopo JNIA, Mohammed Ngayahika alisema lilifanyika kwa kasi na ufanisi mkubwa likihusisha jumla ya lita 98,709 za nishati hiyo.
“Kwa hapa nchini Puma Energy ndio yenye uwezo pekee wa kujaza mafuta kwenye ndege kubwa kutokana na uwekezaji mkubwa iliyoufanya kwenye vifaa vya kisasa vyenye uwezo wa ‘kupump’ mafuta kwa kasi kubwa kama tulivyofanya kwenye zoezi hili ambapo tulisukuma mafuta kwa kasi ya lita 2,800 kwa kila dakika moja na hivyo kufanya zoezi hili kuwa rahisi sana tena kwa ufanisi mkubwa na kwa kuzingatia taratibu zote za kiusalama,’’ alisema.
Naye, Emmanuel Ngowi kutoka kampuni hiyo ambae ndiye aliyeendesha zoezi hilo alisema baada ya kukamilika kwa zoezi hilo Shirika la Ndege la Emirates lilionyesha kuridhishwa kwake na ubora wa huduma hiyo hatua ambayo muhimu katika muendelezo wa biashara. “Kwa muda mrefu Puma Energy tumejenga sifa nzuri katika utoaji wa huduma zetu kutokana na ufanisi wetu, rekodi nzuri katika masuala ya usalama pamoja na bei yenye ushindani,’’. aliongeza
Ndege hiyo iliyopaswa kutua nchini Mauritius , ilitua kwa dharura uwanjani hapo majira ya saa 7:15 mchana ikiwa na abiria 475 kufuatia hali mbaya ya hewa kwenye uwanja ilipotakiwa kutua nchini humo.
Kwa mujibu wa Meneja Idara ya Mafuta ya Ndege wa kampuni hiyo, Raymond Tungaraza alisema hatua hiyo ni sehemu ya uthibitisho kuwa Tanzania kupitia kampuni ya Puma Energy ina uwezo wa kutosha kutoa huduma ya nishati hiyo hata kwa ndege kubwa zaidi duniani.
“Uwezo wa kutoa huduma ya nishati ya mafuta kwa ndege kubwa kama hizi tena kwa ufanisi ni moja ya kivutio muhimu kwa mashirika mengine makubwa kuweza kuleta ndege zao hapa nchini hasa kipindi hiki ambapo Serikali imejipanga kuleta mageuzi katika sekta ya anga hivyo Puma Energy Tanzania tunajivunia kuwa sehemu ya kuwezesha mageuzi hayo,’’ alisema.
Akizungumzia zoezi hilo lililofanyika mapema siku ya Jumatano kabla ndege hiyo haijaondoka hapa nchini kuelekea Mauritius, Meneja wa Kituo cha Mafuta cha kampuni hiyo kilichopo JNIA, Mohammed Ngayahika alisema lilifanyika kwa kasi na ufanisi mkubwa likihusisha jumla ya lita 98,709 za nishati hiyo.
“Kwa hapa nchini Puma Energy ndio yenye uwezo pekee wa kujaza mafuta kwenye ndege kubwa kutokana na uwekezaji mkubwa iliyoufanya kwenye vifaa vya kisasa vyenye uwezo wa ‘kupump’ mafuta kwa kasi kubwa kama tulivyofanya kwenye zoezi hili ambapo tulisukuma mafuta kwa kasi ya lita 2,800 kwa kila dakika moja na hivyo kufanya zoezi hili kuwa rahisi sana tena kwa ufanisi mkubwa na kwa kuzingatia taratibu zote za kiusalama,’’ alisema.
Naye, Emmanuel Ngowi kutoka kampuni hiyo ambae ndiye aliyeendesha zoezi hilo alisema baada ya kukamilika kwa zoezi hilo Shirika la Ndege la Emirates lilionyesha kuridhishwa kwake na ubora wa huduma hiyo hatua ambayo muhimu katika muendelezo wa biashara. “Kwa muda mrefu Puma Energy tumejenga sifa nzuri katika utoaji wa huduma zetu kutokana na ufanisi wetu, rekodi nzuri katika masuala ya usalama pamoja na bei yenye ushindani,’’. aliongeza
Ndege hiyo iliyopaswa kutua nchini Mauritius , ilitua kwa dharura uwanjani hapo majira ya saa 7:15 mchana ikiwa na abiria 475 kufuatia hali mbaya ya hewa kwenye uwanja ilipotakiwa kutua nchini humo.
Mtoa huduma
ya Mafuta ya ndege wa kampuni ya Puma Energy katika Kituo cha Mafuta cha
kampuni hiyo kilichopo Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA)
jijini Dar es Salaam Bw Emmanuel Ngowi akisimamia ujazaji wa mafuta kwenye ndege
kubwa aina ya Airbus 380 inayomilikiwa na Shirika la Ndege la Emirates iliyotua
kwa dharura kwenye uwanja huo hivi karibuni.
Zoezi la
ujazaji mafuta likendelea…!
Kisha
taratibu zote za manunuzi zilifuatwa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...