Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MAKANDARASI, Wasambazaji na wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi nchini wamepatiwa mafunzo yanayohusu ujenzi kwa lengo la kuifahamu vema sekta hiyo yenye ushindani mkubwa.
Mafunzo hayo yametolewa leo jijini Dar es Salaam na
Kampuni ya Imports International Tanzania Ltd ambayo ni waagizaji na wasambazaji wa vifaa vya ujenzi ambapo pia warsha imehusu mafunzo kuhusu matumizi ya vifaa vya drywall gypsum partition and pro-plaster wall finish.
Lengo la mafunzo hayo ni kwa ajili ya kumalizia ukuta kutoka Saint Gobain ambao ndiyo watengenezaji wa vifaa hivyo.Akizungumza kuhusu warsha hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Imports International Tanzania Ltd Trushal Jethwa amesema lengo la mafunzo lilikuwa ni kuwaleta pamoja makandarasi, wasambazaji na wafanyabiashara.
"Lengo ni kuwajulisha kuhusu maendeleo ya hivi karibuni katika sekta ya ujenzi ambayo ina ushindani mkubwa sana. "Katika ulimwengu ambao teknolojia inabadilika haraka sana katika sekta ya ujenzi daima ni muhimu kuwapa wadau baadhi ya maendeleo ya hivi karibuni ili kukua pamoja kama timu, haisaidii sisi kuendelea kuwa na ujuzi Hui bila wajulisha wadau wetu," amesema Jethwa.
Amefafanua mafunzo hayo yanayotolewa na kampuni yao ya Saint Gobain ambao ni wazalishaji wa gyproc ambao wanaamini kuwa aina hiyo ya mafunzo inasisitiza ahadi yao ya kujenga uhusiano mzuri na jamii iliyowazunguka kwa ujumla.
"Hapa leo Saint-Gobain wanatueleza jinsi vifaa vyao vinavyochangia maisha ya kila siku, kwa kupitia bidhaa zake, wanaonesha utaalamu wa vifaa, utamaduni wa ubunifu, ufahamu wa mahitaji ya wateja na mbinu kwa njia ya uwazi na wajibu," amesema Trushal Jethwa.
Ameongeza "Bidhaa za leo zinaonyesha thamani tunayowaletea wateja. Ninataka kila mtu ajue mambo muhimu ambayo Saint-Gobain inasimamia pamoja na nafasi za bidhaa zetu katika maisha ya kila siku.
" Saint Gobain kutokea Ufaransa inapatikana katika nchi zaidi ya 67 duniani kote, mafunzo hayo pia yanatarajiwa kufanyika katika chuo cha Veta na Kariakoo kama sehemu ya uwajibikaji wao wa kijamii," amesisitiza.
MAKANDARASI, Wasambazaji na wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi nchini wamepatiwa mafunzo yanayohusu ujenzi kwa lengo la kuifahamu vema sekta hiyo yenye ushindani mkubwa.
Mafunzo hayo yametolewa leo jijini Dar es Salaam na
Kampuni ya Imports International Tanzania Ltd ambayo ni waagizaji na wasambazaji wa vifaa vya ujenzi ambapo pia warsha imehusu mafunzo kuhusu matumizi ya vifaa vya drywall gypsum partition and pro-plaster wall finish.
Lengo la mafunzo hayo ni kwa ajili ya kumalizia ukuta kutoka Saint Gobain ambao ndiyo watengenezaji wa vifaa hivyo.Akizungumza kuhusu warsha hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Imports International Tanzania Ltd Trushal Jethwa amesema lengo la mafunzo lilikuwa ni kuwaleta pamoja makandarasi, wasambazaji na wafanyabiashara.
"Lengo ni kuwajulisha kuhusu maendeleo ya hivi karibuni katika sekta ya ujenzi ambayo ina ushindani mkubwa sana. "Katika ulimwengu ambao teknolojia inabadilika haraka sana katika sekta ya ujenzi daima ni muhimu kuwapa wadau baadhi ya maendeleo ya hivi karibuni ili kukua pamoja kama timu, haisaidii sisi kuendelea kuwa na ujuzi Hui bila wajulisha wadau wetu," amesema Jethwa.
Amefafanua mafunzo hayo yanayotolewa na kampuni yao ya Saint Gobain ambao ni wazalishaji wa gyproc ambao wanaamini kuwa aina hiyo ya mafunzo inasisitiza ahadi yao ya kujenga uhusiano mzuri na jamii iliyowazunguka kwa ujumla.
"Hapa leo Saint-Gobain wanatueleza jinsi vifaa vyao vinavyochangia maisha ya kila siku, kwa kupitia bidhaa zake, wanaonesha utaalamu wa vifaa, utamaduni wa ubunifu, ufahamu wa mahitaji ya wateja na mbinu kwa njia ya uwazi na wajibu," amesema Trushal Jethwa.
Ameongeza "Bidhaa za leo zinaonyesha thamani tunayowaletea wateja. Ninataka kila mtu ajue mambo muhimu ambayo Saint-Gobain inasimamia pamoja na nafasi za bidhaa zetu katika maisha ya kila siku.
" Saint Gobain kutokea Ufaransa inapatikana katika nchi zaidi ya 67 duniani kote, mafunzo hayo pia yanatarajiwa kufanyika katika chuo cha Veta na Kariakoo kama sehemu ya uwajibikaji wao wa kijamii," amesisitiza.
Mtaalam wa Ujenzi , Member Mashabela akitoa maelezo ya vifaa vya ujenzi kwa wahandisi na wakandarasi waliofika katika ofisi Saint Gobain kuhusiana na ujenzi wa kisasa kwa vifaa vya kisasa leo jijini Dar es Salaam.
Mtaalam wa ufundi wa Saint Gobain Development East Africa, Stanley Katabarwa (Mwenye miwani
Baadhi ya vifaa vya ujenzi
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...