Na Emmanuel Masaka ,Globu ya jamii
MEYA wa Ubungo Boniface Jacob ametembelewa na Mabingwa ngumi za ridhaa ambao wameshinda mataji mbalimbali ya ubingwa pamoja na Medali sita katika Shindano la Mchezo wa Ngumi kwa Mkoa wa Dar es Salaam
yaliyofanyika Uwanja wa Taifa .
Mabondia walioshinda Medali hizo ni Shomari Pendeza kilo 49,Khamisi Maya kilo 69,Mustafa Khalidi kilo 52,Prospa John kilo 60,Frank Lucian kilo 56 na Alex Mshamba kilo 56.
Hivyo imeelezwa leo na Meya Jacob kuwa mabondia wameiletea Manispaa ya Ubungo medali za Dhahabu 1,Shaba 2 na Fedha 3 na hiyo ni heshima kubwa kwa niaba ya vijana wote katika Manispaa ya Ubungo.
Katika neno la Shukrani Meya Jacob amejitolea kuwa Mlezi wa kambi yao ya Shirikisho la Ngumi kwa Wilaya ya Ubungo zilizopo Kimara.
Pia ameahidi kuwatafutia udhamini wa mchezo huo wa ngumi ambapo pia amewaeleza kuwapatia pair za Gloves,boxing pad,Punching Bags,Clip bandage,Head protectors,na Boxing gears zingine.
Meya wa ubungo Boniface Jacob akiangalia medali za Dhahabu alizoshinda mabondia Mabingwa wa ngumi za ridhaa, ambapo amejitolea kuwa mlezi wa kambi ya Shirikisho la ngumi wilaya ya Ubungo mkoa wa Dar es Salaam.
Meya wa ubungo,Boniface Jacob (wapili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mabondia wa ngumi za ridhaa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...