*Azungumzia miradi mipya 109 waliyoisajili kwa kipindi cha miezi minne,fursa za ajira

Na Said Mwishehe,Globu

MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) Geoffrey Mwambe ametoa hakikisho kwa wawekezaji na Watanzania kwa ujumla kuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi kubwa na kwa sasa nchi yetu inashika nafasi ya tano kati ya mataifa 10 duniani ambayo uchumi wake unakuwa kwa kasi.

Amesema kuimarika kwa uchumi huo wa Tanzania na kukuwa kwa kasi, maana yake inatoa usalama kwa anayetaka kuwekeza nchini kuwa na uhakika wa mtaji wake huku akielezea mafanikio ya TIC katika kuhamasisha uwekezaji nchini ambapo kuanzia Januari hadi Aprili mwaka huu wamefanikisha kuandikisha miradi mipya 109 inayotarajia kutoa fursa ya ajira 18,172.

Mwambe amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anatoa mafanikio ya TIC kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Aprili mwaka huu ambapo amefafanua kutokana na matokeo hayo ya haraka ya ukuaji wa uchumi yametokana na jitihada za Serikali  chini ya Rais Dk.John Magufuli katika kupambana na rushwa , kuondoa urasimu kwa kutengeneza mazingira wezeshi ya usajili wa biashara na leseni kwa wawekezaji wa nfani na nje.

Akifafanua zaidi mambo mengine ambayo yamefanyika katika kuwahudumia wawekezaji kwa haraka ni pamoja na kuboresha mfumo wa huduma mahala pamoja ndani ya TIC ambapo kwa sasa kuna maofisa zaidi  10 wanaotoka kwenye wizara,idara na taasisi za Serikali kwa ajili ya kutoa huduma za kusajili kampuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...