Na Leandra Gabriel, blogu ya jamii

NAIBU  Waziri Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa Mkuranga, Abdalah Ulega ameweka jiwe la msingi  kwa ajili ya  ujenzi wa madaraja matatu wilayani Mkuranga mkoani Pwani

Akizungumzia ujenzi wa madaraja hayo ,Ulega ameeleza  madaraja hayo matatu yatajengwa katika vijiji vitatu ambavyo ni  Tamabani Mwanabilatu, na Kifaurongo.

Amesema ujenzi wa madaraja hayo hadi kukamilika kwake Julai mwaka huu utagharimu kiasi cha takribani Sh.bilioni 1.5.Aidha Ulega amemuagiza mkandarasi anayejenga madaraja hayo asichukue vibarua wa kutoka sehemu nyingine bali wachukuliwe katika vijiji ambavyo mradi huo wa ujenzi wa madaraja unafanyika ili wakazi wa maeneo hayo wapate vipato.

Pia Ulega  amewaomba wananchi wa Wilaya ya Mkuranga kushirikiana na wakandarasi wa ujenzi ili kuweza kurahisisha kazi hiyo na kufanya mradi huo kuisha kwa wakati.Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini(TARULA) Wilaya ya  Mkuranga, Mhandisi Emmanuel Mubofu amesema miradi hiyo ita kamilika ndani ya miezi miwili tu, yaani kuanzia mwezi Mei hadi Julai mwaka huu.

Mubofu ameeleza  mradi huo umeanza na kufikia Agosti wananchi wataanza kutumia madaraja hayo licha ya kuikamilisha Julai.Kuhusu  fedha za ujenzi Mubofu ameeleza kuwa zimetoka mfuko wa barabara kwa ajili ya kero hizo za kimiundombinu zilizokuwa zinawakabili wakazi hao.

Aidha ameeleza wakandarasi wawili wameshaanza kazi na kwa asilimia 20 tayari ujenzi umekamilika.
 Naibu Waziri Mifungo na Uvuvi,Mbunge wa Mkuranga  Abdallah Ulega (watatu kutoka kulia) akiweka  jiwe la msingi  kwa ajili ya  ujenzi wa madalaja mitatu yatakayogharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.5
 Naibu Waziri Mifungo na Uvuvi, Mbunge wa Mkuranga,Abdallah Ulega akizungumza na wanaichi wa kijiji cha Kifaurongo kabla katika hafla ya kuweka  jiwe la msingi  kwaajili ya  ujenzi wa madalaja mitatu yatakayogharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.5(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii)
 Naibu Waziri Mifungo na Uvuvi, Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega  akimsikiliza Kaimu Mejeneja Tarula Mkuranga Muhandisi Emmanuel  Mubofu alienyosha mkono alipo tembelea mradi wa ujenzi wa madaraja.
 Naibu Waziri Mifungo na Uvuvi,Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akiwa ameambatana na  viongozi wa (CCM) wa Wilaya Mkuranga  wakivuka Mto Mzinga.
Wananichi wa kijiji cha Kifaurongo wakivuka Mto Mzinga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...