Na Dixon Busagaga, Moshi.
MSANII wa Sanaa za Uchongaji Vinyago Bw. Athumani Mwariko ametoa Kinyago cha Kiafrika kama zawadi kwa Rais wa Urusi ,Vladimir Putin ikiwa ni zawadi kwa nchi hiyo kuandaaa na kufanikisha fainali za Fifa za Kombe la Dunia.
Mwariko ambaye pia ni Mkurugenzi wa taasisi ya Sanaa ya Kilimanjaro Cultural Heritage Centre ya mkoani Kilimanjaro alisema zawadi hiyo itawasilishwa kwa Rais Putin kupitia kwa Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe.

Akizungumza na wanahabari, Bw. Mwariko alisema zawadi hiyo kwa Rais Putin inatokana na uandaaji mzuri wa mazingira uliopelekea kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa fainali hizo zilizomalizika hivi karibuni katika miji mbalimbali nchini Urusi.
“Michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu tumeweza kushuhudia mazingira tofauti kattika maandalizi yake ,kufanyika hadi kumalizika kwake ,fainali za mwaka huu zimekuwa na utofauti mkubwa sana ukilinganisha na zile zilizopita,”alisema Mwariko.
MSANII wa Sanaa za Uchongaji Vinyago ,Athumani Mwariko akiwa na Kinyago chake alichokichinga. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...