Siku ya Sita ya ziara ya Waziri
Makamba imemfikisha Mkoani Geita, Wilayani Chato katika Kijiji cha
Nyamirembe ambapo pamoja na mambo mengine Mhe. Makamba ametembelea
Kisiwa cha Magafu na kuahidi kutuma timu ya wataalamu kwa ajili ya
kufanya tathmini ya namna ya kulinda kisiwa hicho kwa mujibu wa Sheria
ya Mazingira ya mwaka 2004, ikiwa ni eneo tengefu kwa mazalia ya samaki.
Akiongea na Uongozi wa Mkoa wa Geita Waziri Makamba amesema kuwa jitihada za Serikali ni pamoja na kuhakikisha ulinzi madhubuti kwa kisiwa hicho ili kiwe kielelezo cha mandhari tulivu kwa mazalia ya samaki na bioanuai.
Waziri Makamba amesema kuwa hakuna sekta yoyote muhimu kwa uchumi wa nchi isiyohitaji Hifadhi ya Mazingira hivyo Sheria ya Mazingira kifungu namba 51 inatoa mamlaka na nafasi ya kulinda maeneo nyeti na kuainisha kuwa kuna dhana potofu kuwa uhifadhi wa mazingira ni kinyume na maendeleo.
Dhana ya uhifadhi inaendana na utashi, uwezo, utayari na ushirikishwaji wa wananchi wenyewe. “Tunapoongelea uhifadhi tunaamanisha, kuweka utaratibu wa kutumia maeneo yaliyopendekezwa kuhifadhiwa kwa taratibu zitakazopendekezwa, mfano kama tunahifadhi kisiwa, tutaweka utaratibu maalumu wa uvuaji wa samaki katika eneo hilo” Makamba alisisitiza.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akizungumza na wakazi wa kijiji cha Nyamirembe juu ya utayari wao wa kuhifadhi mazingira ya Kisiwa hicho ili kuwa miongoni mwa maeneo yanayopendekezwa kulindwa kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira. 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akikagua maeneo ya Kisiwa cha Magafu, takribani mwendo wa dakika thelathini kutoka mwalo wa Nyamirembe. Waziri Makamba aheahidi kutuma wataalamu ili kujiridhisha zaidi kabla ya kutanga katika gazeti la Serikali.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akikagua maeneo ya Kisiwa cha Magafu, takribani mwendo wa dakika thelathini kutoka mwalo wa Nyamirembe. Waziri Makamba aheahidi kutuma wataalamu ili kujiridhisha zaidi kabla ya kutanga katika gazeti la Serikali.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...