Na Agness Francis,blogu ya Jamii.

Kikosi cha Mbeya city chatamba kufanya vizuri katika mchezo wao dhidi ya mnyama Simba sc hapo kesho katika muendelezo wa michuano ya Ligi kuu Tanzania bara.

Mpambano huo utakao tifulia katika dimba la Uwanja wa Taifa huku Mbeya city wakiwa wageni wa mchezo huo.Mechi ya kwanza Mbeya city ilipata kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa wana lamba lamba Azam fc katika dimba la Azam complex Chamazi,ambapo simba alishinda 1-0 dhidi ya Prisons.

Lakini katika kuelekea mtanange huo dhidi ya mabingwa watetezi Simba,kikosi cha Mbeya city imejihakikishia kutorudia makosa waliyoyafanya katika mchezo uliopita 

"Kambi ipo salama vijana wanajituma kwa kuwa tunajua tumekosea wapi tunafanyia kazi makosa tunarekebisha pale tulipokosea ili tuweze kufanya vizuri gemu inakuja dhidi ya Simba,hatuturudia tena makosa tuliyoyafanya"amesema kocha msaidizi Josiah Steven. 

Meneja wa Mbeya city Deo Julias amesema vijana wanamorali ya kufanya vizuri kuhakikisha wanapata ushindi na kurudi nyumbani wakiwa na pointi 3.
Kikosi cha Mbeya City.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...