
Sehemu
ya Wafanyakazi wa Kampuni ya EY Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja
baada ya kumalizika kwa Bonanza lao la Michezo, lililofanyika mwishoni
kwa wiki kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM). Zaidi
ya michezo kumi ilichezwa uwanjani hapo, Wafanyakazi hao walijigawa
katika makundi matano kutokea kila kitengo na kutengeneza timu tano
katika kila mchezo (Kilimanjaro, Tigers, Rockets, Eagles pamoja na
Wolves), ambapo ushindi wa jumla ulinyakuliwa na Timu Kilimanjaro.
Mtendaji
Mkuu Mwenza wa Kampuni ya EY Tanzania, Ukaguzi wa Hesabu (Audit
Partner), Neema Kiure Mssusa akingumza wakati wa ufunguzi wa Bonanza la
Michezo kwa Wafanyakazi wa Kampuni hiyo, lililofanyika mwishoni kwa wiki kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM).
Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya EY Tanzania wakichuana vikali katika mchezo wa Soka wakati wa Bonanza lao la Michezo, lililofanyika mwishoni kwa wiki kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM).





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...