*Wamo wakuu wa wilaya,mikoa na mawaziri,awataka waheshimu mamlaka nyingine
*Aahidi kuandika barua kwa Kamishna wa TRA,aeleze namna wanavyowatafuta wawekezaji

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MGURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) Geoffrey Mwambe amewataka viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwamo baadhi ya wakuu wa wilaya,wakuu wa mikoa na mawaziri kuacha kutoa matamko na maagizo kwa wawekezaji nchini.

Amesema ni vema kila mamlaka ikatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na kufafanua iwapo kuna tatizo lolote likiwemo la kodi,vibali au bora wa bidhaa kwa muwekezaji yoyote kuna haja ya kufuata taratibu wa kutafuta ufumbuzi kupitia mamlaka husika badala ya kutolewa maagizo ambayo hazingatii sheria.

Mwambe amesema hayo leo jijini Dar es Saalam wakati anazungumzia ziara ambayo TIC pamoja na wadau wanaohusika na sekta ya uzalishaji dawa na vifaa tiba nchini ambayo waliifanya Korea Kusini na China, ushiriki wao katika Maonesho ya Nanenane pamoja na kueleza majukumu yao ya kuelimisha umma na  kuhamasisha uwekezaji.

Hivyo ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa  kuna wimbi la viongozi  kutoa maagizo na matamko na hasa yanayohusiana na masuala ya kikodi,vibali na mambo mengine.Amesema kwamba TIC  wanafanya kazi kubwa na ngumu ya kuhamasisha wawekezaji na mitaji kuja nchini na wanatumia gharama katika kufanikisha

"Kama kuna muwekezaji yoyote ana tatizo lolote wa kufahamishwa ni kituo cha wawekezaji.Ni jambo la kushangaza Mkuu wa Wilaya anatoa makadirio ya kodi, anatoa siku mbili kodi ilipwe wakati sheria haiko hivyo.

" Unapozungumzia suala la kodi kuna utaratibu wake na sheria zake,hivyo iwapo kuna tatizo la kikodi kwa muwekezaji kiongozi wasiliana na mamlaka husika watatafuta ufumbuzi wake."Kama ni suala la vibali wapo wanaohusika na vibali kwa ajili ya wawekezaji,hivyo fuata utaratibu badala ya kutoa maagizo wakati huna mamlaka ya kufanya hivyo," amesema.

Ameongeza kwamba viongozi wote jukumu lao ni kutoa taarifa kwa mamlaka husika na si kutoa maagizo na miongozo bila kufuata taratibu.Ametoa mwito kwa viongozi wote kushirikiana na TIC katika kuhakikisha wanaendelea kuweka uaminifu kwa wawekezaji ili kifikia uchumi wakati.Pia ameomba ngazi zote za kimamlaka kila mmoja kusimama katika mipaka yake kwani kila mmoja yupo kisheria na sababu za kueleza hayo ni kukumbusha wajibu wa kila taasisi kutekeleza majukumu yake bila kuingia mipaka ya mwingine.


Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji TIC Bw. Geoffrey Mwambe akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya ofisi hizo jijini Dar es salaam leo wakati alipozungumzia kuhusu Viongozi mbalimbali wa serikali wakiwemo wakuu wa wilaya, Wakurugenzi, Wakuu wa mikoa na Mawaziri wanaotoa matamko kuhusu wawekezaji hapa nchini.
Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji TIC Bw. 
Geoffrey  Mwambe akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya ofisi hizo jijini Dar es salaam leo. Alipozungumzia kuhusu Viongozi mbalimbali wa serikali wakiwemo wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Wakuu wa mikoa na Mawaziri wanaotoa matamko kuhusu wawekezaji hapa nchini.

Waandishi wa habari na wakuu wa vitengo mbalimbali kutoka kituo cha Uwekezaji TIC wakimsikiliza Mkurugenzi wa Kituo cha hicho Bw. 
Geoffrey  Mwambe akizungumza leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...