Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Uvinza Mhe. Mwanamvua Mlindoko, wakati alipowasilia wilayani Uvinza Tarafa ya Nguruka mkoani Kigoma Jana 24/10/2018, kwa lengo la kuzungumza na wananchi kufuatia tukio la kushambuliwa na kuuawa kwa askari wawili na wingine mmoja kujeruhiwa wakati wakitekeleza zoezi la kuwaondoa wananchi waliovamia eneo la Ufugaji Ranchi ya Taifa NARCO kwa kuendesha shughuli za kilimo kinyume cha sheria na taratibu za nchi. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akizungumza na wananchi (hawapo Pichani) wa Tarafa ya Nguruka wilayani Uvinza mkoani Kigoma Jana 24/10/2018, na kuwataka kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kufichua uhalifu na wahalifu pamoja na watu wanaojihusisha na matukio ya mauaji ili waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akiondoka baada ya kumaliza mkutano na wananchi wa Tarafa ya Nguruka wilayani Uvinza mkoani Kigoma Jana 24/10/2018, ambapo IGP Sirro, aliwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa sahihi zitakazofanikisha kukamatwa kwa watu waliojihusisha na tukio la kuwashambulia na kuwaua askari wawili na wananchi wawili wilayani humo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akiondoka baada ya kumaliza mkutano na wananchi wa Tarafa ya Nguruka wilayani Uvinza mkoani Kigoma Jana 24/10/2018, ambapo IGP Sirro, aliwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa sahihi zitakazofanikisha kukamatwa kwa watu waliojihusisha na tukio la kuwashambulia na kuwaua askari wawili na wananchi wawili wilayani humo. Picha na Jeshi la Polisi.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...