Na Mwandishi wetu
BONDIA Issa Nampepeche na Hashimu Chisola wamepima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa raundi kumi utakaofanyika jumamosi ya Octobar 20 katika ukumbi wa CCM Mwijuma Mwananyamala akizungumza wakati wa upimaji mratibu Ibrahimu Kamwe 'BigRaght' 

amesema kuwa siku hiyo kutakuwa na mapambano mbalimbali ya kukata na shoka kwani wamejipanga kuinua mchezo wa masumbwi katika kitongoji cha mwananyamala na viunga vyake

mbali na pambano hili siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine ya kukata na shoka kati ya Shabani Madilu atakaezipiga na Selemani Bangaiza na bondia machachari anaekuja kwa kasi ya ali ya juu Hamisi Maya atazipiga na Zumba Kukwe kutoka Kibaha Mkoa wa Pwani mpambano mwingine utawakutanisha Mbena Rajabu atakae oneshana umwamba na Fredy Masinde na Josephe Mbowe atazikunja na Mwinyi Mzengela 

aliongeza kwa kusema BigRight Sports and Arts Promotion imejizatiti kuinua vipaji vya mabondia chipkizi na kuwaendeleza wale walio katika chati ya juu kwa kuwandalia mapambano mbalimbali yakiwemo ya ubingwa wa taifa na yale ya ubingwa wa kimataifa

siku hiyo pia kutakuwa zikiuzwa DVD mpya za masumbwi ambazo zinaonesha mafunzo mbalimbali ya mchezo wa ngumi yanavyoanza hatua kwa hatua mpaka kujua kitu kamili katika mchezo huo pia kunakuwa na mapambano ya mabondia mabigwa wa dunia wa mchezo huo kama Floyd

Maywether, Manny Paquaio,mike Tyson, Mohamed Alli pamoja na mabambano ya ngumi ya ndani zilizo taharishwa na kocha maili wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye anajishughulisha na uzaji wa vifaa mbalimbali vya ngumi nchini kama vile Glove gumshirt clip bandeji bukta protecter na vifaa vingine.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...