NA MWAMVUA MWINYI, PWANI 

KAMANDA wa polisi mkoani Pwani (ACP) Wankyo Nyigesa ameweka bayana, askari wa usalama barabarani hawataona muhali kuchukua hatua dhidi ya mabasi ya abiria yatakayojaza abiria pamoja na yanayokalisha abiria waliozidi kwenye ndoo za lita 20. 

Aidha ameyaasa ,magari ya watoto wa shule mengi ni machakavu hivyo ameelekeza wayapeleke yakaguliwe kabla ya kubeba wanafunzi . 

Akitoa rai hiyo kwa waandishi wa habari, Nyigesa alisema ,haiwezekani madereva wakakiuka sheria za usalama barabarani kwa makusudi wakitegemea kutoa faini bali wanachotakiwa ni kufuata sheria zilizopo. 

Aliwataka ,abiria na jamii kutoa ushirikiano kwa askari hao kwa kutoa taarifa ama kuyafichua magari ya abiria yanayojaza abiria kupita kiasi ili wayachukulie hatua ikiwemo kupigwa faini. 

Nyigesa alieleza, magari ya watoto wa shule mengi ni machakavu hivyo ameelekeza wayapeleke yakaguliwe kabla ya kubeba wanafunzi . Aliwataka, waendeshaji wa vyombo vya moto kutii sheria, na kwamba magari yao yatakaguliwa yawapo ndani ya mkoa huo. 

“Magari ya watoto yaliyo mengi hayana mikanda sasa ni jukumu lao kujikaguwa kabla hawajakaguliwa na kukamatwa , “Hakuna polisi atakayemuonea aya dereva wala hatutaona muhali katika suala hili la kudhibiti ajali”alisisitiza Nyigesa. 

Kamanda huyo alieleza, kila mmoja atii sheria bila kushurutishwa


Kamanda wa polisi mkoani Pwani (ACP) Wankyo Nyigesa, akizungumza na wanahabari (hawapo pichani)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...