Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
MSANII wa Muziki wa Kughani na Kiongozi wa Mjomba Bendi, Mrisho Mpoto amesema kampeni ya Kitaifa ya Usafi wa  Mazingira na uhamasishaji wa ujenzi wa Vyoo bora iliyoanza mkoani Tanga katika Wilaya ya Muheza imeweza kubadilisha jamii ya wilaya hiyo kwa kiasi kikubwa.

akizungumza na Michuzi Media Mpoto amesema kuwa sote kwa umoja wetu kama Mjomba Bendi tumedhamiria kila jamii tutakoyoifikia inabdilika kwa kuwa na choo bora ambacho kitasadia kutunza na Mazingira hili kuepukana na magonjwa ya Mlipuko yanayotokana na kujisaidia hovyo.

"Sote kwa pamoja na umoja wetu Watnzania tudumishe uzalendo na kuhakikisha tunalinda afya zetu na familia kwa kuwa na vyoo vilivyobora kwa kuambiana ukweli kuwa 'tusichukulie poa nyumba ni choo"amesema Mpoto.

Mpoto amesema kuwa hakuna Raha Kubwa kama kuwa na nyumba yenye choo bora ambayo unasikia furaha kumkaribisha mgeni pindi anpohitaji kwenda msalani kuliko vile mtu anaomba kwenda msalani alafu unashikwa na kigugumizi.
Msanii wa Muziki wa Kughani na Kiongozi wa Mjomba Bendi Mrisho Mpoto akzingumza na Wakazi wa Kata ya Tingeni Wilayani Muheza Mkoani Tanga ambapo mrsho mpoto ameweza kufikisha ujumbe wa ujenzi wa Choo Bora kwa wakzi wa kata hiyo ambao wamehamsika kuwa na kuta nne za choo kwa kila nyumba kwa kuungna nae kuwa 'Usichukilie Nyumba ni Choo'
Mkuu wa Wilaya ya Muheza akiwasalimia wakazi wa Wilaya hiyo ambao wamefika kusikiliza kampeni ya Nyumba ni choo inayoongozwa na Mrosho Mpoto
 Wasanii wa Mjomba Bendi , Ismail na Nuruelly wakiwatumbuiza wakazi wa Muheza katika Kampeni ya Wizara ya Afya Msichukulie Poa Nyumba ni Choo.
 Sehemu ya Wakazi wa Kata ya Tingeni Wilaya ya Muheza wakifatilia Kampeni ya Nyumba ni Choo inayoendeshwa bendi ya Mjomba chini ya mrisho Mpoto
 Sehemu ya Wakazi wa Kata ya Tingeni Wilaya ya Muheza wakifatilia Kampeni ya Nyumba ni Choo inayoendeshwa bendi ya Mjomba chini ya mrisho Mpoto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...