Na Ripota Wetu,Globu ya jamii
TRENI inayotoa huduma za usafiri kati ya Stesheni ya Dar es Salaam na Pugu Stesheni imepata ajali leo Novemba 2,2018 eneo la Karakata baada ya behewa mbili kuanguka.
Kwa mujibu baadhi ya abiria waliokuwa kwenye treni hiyo wamesema ajali hiyo imetokea leo kwenye saa moja kasoro asubuhi ambapo baada ya kufika eneo hilo mabehewa mawili yalipinduka.
Mmoja wa abiria hao aliyejitambulisha kwa jina la Juma Jebe amesema yeye alikuwa behewa la nne kutoka mabehewa yaliyoanguka na kwamba baada ya tukio hilo kuna baadhi ya abiria walionekana kuzimia kutokana na hofu. Hata hivyo amesema anashukuru kwani hakushuhudia mtu yoyote kuumia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...