Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

TRENI inayotoa huduma za usafiri kati ya Stesheni ya Dar es Salaam na Pugu Stesheni imepata ajali leo Novemba 2,2018 eneo  la Karakata baada ya behewa mbili kuanguka.

Kwa mujibu baadhi ya abiria waliokuwa kwenye treni hiyo wamesema ajali hiyo imetokea leo kwenye saa moja kasoro asubuhi ambapo baada ya kufika eneo hilo mabehewa mawili yalipinduka.

Mmoja wa abiria hao aliyejitambulisha kwa  jina la Juma Jebe amesema yeye alikuwa behewa la nne kutoka mabehewa yaliyoanguka na kwamba baada ya tukio hilo kuna baadhi ya abiria walionekana kuzimia kutokana na hofu. Hata hivyo amesema anashukuru kwani hakushuhudia mtu yoyote kuumia. 

Michuzi Blog itaendelea kukujuza kilichosababisha kuanguka kwa mabehewa hayo baada ya mamlaka husika kuzungumzia.



Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wakitazama ajali ya kuanguka kwa mabehewa ya treni leo asubuhi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...