Na Richard Mwaikenda, Kibiti.

TAASISI ya Namaingo, imezindua uwekezaji wa Mradi wa Mizinga ya nyuki wa asali 55000 wa wanachama wake katika Kijiji cha Kikale, wilyani Kibiti, Mkoa wa Pwani.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo uliofanyika jana kijiji hapo, Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya Namaingo, Ignus Augustino, alisema mipango yao ni kila mwanachama kuwa atamiliki mizinga 50.

Uzinduzi huo ulifanywa mbele ya wananchama waliotoka Dar es Salaam pamoja na wanakijiji wa Kikale katika mabanda matatu yenye mizinga 200 ya kuanzia. Mizinga hiyo ipo ndani ya msitu wa miti ya mikoko inayoaminiwa kutoa daraja la kwanza la asali yenye kiwango cha kimataifa.

Augustino alisema kuwa wamejiandaa vilivyo kuutekeleza mradi huo mkubwa ambapo hivi sasa tayari watalaamu wa kutengeneza malkia wapo eneo la mradi. Urinaji ukianza baada ya miezi sita Kila mzinga utakuwa unatoa kilo 20 za asali. Naye Mwenyekiti Msaidizi wa Namaingo, Elesia Mkuru, alisema baadhi ya wanachamama walikuwa 

hawaamini kuwa mradi huo utandinduliwa, lakini sasa wameshaona ukweli wa mambo.Aliipoongeza Serikali kupitia Wakala wa Misitu Tanzania (TFS), kwa kuwaruhusu kuwekeza mradi huo katika misitu iiyopo mikoa ya Pwani, Iringa, Njombe, Dar es Salaam na Morogoro. Mwanachama wa Namaingo, Queen Ryoba, alisema kuwa wamefurahi sana kuona mradi huo umeanza 
Baadhi ya Wanachama wa Taasisi ya Namaingo wakiangalia moja kati ya mabanda ya ufugaji nyuki wa asali wakati wa uzinduzi Mradi wa Mizinga 55000 katika Kijiji cha Kikale, wilayani Kibiti, Mkoa wa Pwani.PICHA NA RICHARD MWAIKENDA.
Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya Namaingo, Ignus Augustino, akiwaongoza wanachama kuangalia mizinga.
Wanachama wakiangalia baadhi ya mizinga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...