*Akuta baadhi ya wakandarasi wanasuasua, wengine wako vizuri
*Aitisha kikao cha Mawaziri, Makatibu Wakuu wote kesho saa 5 asubuhi
*Ataka leo jioni apewe taarifa ya kila taasisi inayohusika Ihumwa
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amekagua ujenzi wa eneo la Mji wa Serikali
lililoko Ihumwa na kubaini kuwa baadhi ya wakandarasi hawaendi na kasi
inayotarajiwa na Serikali.
Waziri
Mkuu ameamua kuitisha kikao cha Mawaziri wote na makatibu wakuu wote
kesho (Ijumaa) saa 5 asubuhi ili waeleze kazi hiyo itakamilishwa lini.Ametoa agizo kauli hiyo leo mchana (Alhamisi, Desemba 27, 2018) mara
baada ya kukagua ujenzi wa ofisi za wizara zote pamoja na Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika eneo la Mtumba lililoko km. 17
kutoka jijini Dodoma.
“Nimekagua
maeneo yote na kukuta baadhi ya wakandarasi wanatakiwa kujenga majengo
ya wizara nne hadi tano. Sijaridhika na baadhi ya kazi, nimeitisha kikao
cha Mawaziri wote kesho ili tuangalie ni mkandarasi yupi anaweza kumudu
hii kazi.”
“Nimebaini
kuna tatizo kubwa la upatikanaji wa vifaa vya ujenzi kama kokoto,
nondo, matofali na kikao cha kesho kitahusisha Mawaziri, Makatibu Wakuu,
viongozi wa Mkoa na Jiji la Dodoma, wakandarasi wote ili tukubaliane
kazi hii inaisha lini,” amesema.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisoma ramani ya Mji wa Serikali wakati
alipokagua Ujenzi wa mji huo, eneo la Ihumwa jijini Dodoma, Desemba 27,
2018. Wengine pichani kutoka kushoto ni Afisa Mipango Miji katika jiji
la Dodoma, William Alfayo, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,
Vijana na Ajira, Anthony Mavunde, Mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin
Kunambi na Kulia ni Katibu wa Kikosi Kazi cha Kuhamishia Shughuli za
Serikali jijini Dodoma, Meshack Bandawe.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Katibu wa Kikosi Kazi
cha Kuhamishia Shughuli za Serikali jijini Dodoma, Meshack Bandawe
kuhusu Ujenzi wa Mji wa Serikali wakati alipokagua Ujenzi huo, eneo la
Ihumwa jijini Dodoma, Desemba 27, 2018.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua Ujenzi wa jengo Ofisi ya Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati
alipokagua Ujenzi wa Mji wa Serikali katika eneo la Ihumwa jijini
Dodoma, Desemba 27, 2018.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama kazi ya kusuka nondo kwa ajili ya
nguzo za jengo la Ofisi za Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakati alipokagua Ujenzi wa Mji wa
Serikali, eneo la Ihumwa jijini Dodoma, Desemba 27, 2018. Kulia kwake
ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Anthony
Mavunde.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua Ujenzi wa Msingi wa jengo la Ofisi za
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wakati alipokagua Ujenzi wa
Mji wa Serikali, eneo la Ihumwa jijini Dodoma, Desemba 27, 2018. (Picha
na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...