Na Veronica Simba – Geita
Wizara ya Nishati inatekeleza mkakati wa kuwaunganishia umeme wa uhakika wachimbaji wadogo wa madini kote nchini, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais John Magufulu kuiwezesha sekta hiyo izalishe kwa tija kwa manufaa yao binafsi na ya Taifa kwa ujumla.

Akizungumza katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi wa kiwanda cha kuchenjua dhahabu, kinachomilikiwa na kampuni ya Padalu, kijijini Lumasa, Chato; Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa eneo hilo, Dkt Medard Kalemani, alisema serikali imefunga transfoma tano zenye uwezo wa KVA 400 hadi 1,000 ili kuwawezesha wachimbaji wadogo wa Geita kuzalisha kwa tija.

“Umeme huu mkubwa utawawezesha wachimbaji kuchimba , kuchenjua na kuongeza thamani dhahabu yao ili kuiongezea thamani, iwapatie faida na waweze kulipa kodi na mrabaha serikalini,” alisema.

Akieleza zaidi, Waziri Kalemani alisema yako maeneo mkoani humo ambayo bado hayajafikiwa na huduma hiyo lakini akabainisha kuwa utaratibu wa kufunga transfoma nyingine tano zenye uwezo uleule, unafanyika ili kuyafikia maeneo ya wachimbaji yaliyosalia ikiwemo Mbogwe na Nyakafuru.
 Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani (kushoto) na Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (kulia), wakifungua kitambaa maalum kilichofunika jiwe la msingi la kiwanda cha uchenjuaji dhahabu cha Padalu, kilichopo Chato Geita, kuashiria uzinduzi rasmi. Hafla hiyo ilifanyika Januari 2, 2019.
 Msimamizi wa Kiwanda cha kuchakata dhahabu cha Padalu, kilichopo Chato Geita, Abel Lucas (kulia), akitoa maelezo jinsi kinavyofanya kazi kwa Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani pamoja na Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko, na ujumbe waliofuatana nao, wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi wa kiwanda hicho, Januari 2, 2019.
 Msimamizi wa Kiwanda cha kuchakata dhahabu cha Padalu, kilichopo Chato Geita, Abel Lucas (kushoto), akitoa maelezo jinsi kinavyofanya kazi kwa Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani (wa kwanza kulia) pamoja na Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko (wa pili – kulia), wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi wa kiwanda hicho, Januari 2, 2019.
 Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani (katikati), akisalimiana na Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko (kushoto), walipowasili kwenye hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Padalu kilichopo Chato Geita, Januari 2, 2019. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhandisi Msafiri Mtemi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
 Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani akizungumza na wananchi, wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Padalu kilichopo jimboni mwake, Chato Geita, Januari 2, 2019.
Sehemu ya umati wa wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Chato, Dkt Medard Kalemani (hayupo pichani), wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Padalu kilichopo jimboni humo, Chato Geita, Januari 2, 2019.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...