Mshindi wa bodaboda ya biko na sh milioni moja, Deogratius Ngunyale, wa Kinondoni jijini Dar es Salaam ambaye pia ni daktari wa Hospitali ya Muhimbili, (katikati) akiwa na watu wake wa karibu katika makabidhiano ya bodaboda hiyo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki, jijini Dar es Salaam. Droo nyingine kubwa ya biko hufanyika kila Jumatano na Jumapili. Picha na mpigapicha wetu.
Daktari wa Hospitali ya Muhimbili, Dkt Deogratius Patrick Ngunyale, amefanikiwa kukabidhiwa bodaboda yake na sh milioni moja aliyoshinda kutoka kwenye bahati nasibu ya biko iliyochezeshwa jana jumapili, jijini Dar es Salaam na daktari huyo mwenye maskani yake Kinondoni, jijini hapa akiibuka kidedea katika droo hiyo.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Mratibu Msaidizi wa Matukio wa biko, Hassan Ahmed.

Akizungumzia ushindi wake huo, dokta Patrick alisema kushinda bodaboda ya biko kutarahisisha maisha yake kwa kuhakikisha kuwa anaitumia katika mambo mbalimbali ya kukuza uchumi wake.

Kucheza Biko ni kuanzia sh 500 na sh 1000 na kuendelea, huku ushindi wake ukianzia sh 1000 hadi sh 100000 kwa watakaocheza sh 500 hadi sh 9500 wakati watakaocheza kwa sh 1000 na kuendelea, mchezaji anaweza kujishindia zawadi ya papo kwa hapo kuanzia sh 5000 hadi sh milioni moja bila kusahau wote kuingia kwenye droo kubwa ya Jumatano na Jumapili.

Bahati nasibu ya Biko inachezwa kwa mitandao ya simu minne ambayo ni Tigo Pesa, M-Pesa, Artel Money na HaloPesa, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba 2456, huku Watanzania wakiweza kujishindia zawadi kubwa katika droo kubwa za Jumatano na Jumapili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...