Muogeleaji wa klabu ya Bluefins Husain Hassanali akichapa maji katika mashindano ya Taliss-IST. Husain ni miongoni mwa waogeleaji watakao shindana katika mashindano ya Isamilo.

Na Mwandishi wetu

Dar es Salaam. Klabu inayokuja juu kwa kasi katika mchezo wa kuogelea nchini, Bluefins imetangaza kikosi cha waogeleaji 29 kwa ajili ya kushindana katika mashindano ya  Isamilo yaliyopangwa kuanza ijuu mkoani Mwanza.

Muasisi na Kocha Mkuu wa timu hiyo, Rahim Alidina aliwataja waogeleaji  wa kile kuwa ni Alexis Misabo, Filbertha Demello, Maryam Ipilinga, Viva Pujari, Sarah Shariff, Aminaz Kachra, Fatema Manji, Muskan Gaikwad, Aliyana Kachra, Zainab Moosajee na Lina Goyayi.

Waogeleaji wa kiume ni Moiz Kaderbhai, Idris Zavery, Sahal Harunani, Isaac Mukani, Enrico Barretto, Zac Okumu, Hassan Harunani, Mohamedhussein Imran, Husain Hassanali, Burhanuddin Mustansir na Ayaan Shariff.

Wengine ni Kaysan Kachra, Parth Motichand, Shuneal Bharwani, Sahil Chudasama, Salman Yasser, Christian Fernandes na Revocatus Josephat.

 Alidina alisema kuwa wamewajumuisha waogeleaji wenye umri wa miaka  saba (7) kwa lengo la kuwapa uzoefu wa mashindano kabla ya kushindana katika mashindano ya Taifa yaliyopangwa kufanyika  mwezi Aprili.

Alisema kuwa waogeleaji hao wapo katika maandalizi ya mwisho na wanatarajia kuondoka jijini kabla ya Ijumaa ya wiki hii kwenda kuonyesha uwezo wao.

“Haya ni mashindano ya tatu kwa mwaka huu, tulianza na Morogoro na baadaye Taliss-IST. Yote hayo tumefanya vizuri,” alisema.

Alisema kuwa wanatarajia kufanya vyema katika mashindano hayo pamoja na waogeleaji wao kuweka muda mpya wa kuogelea (PBS).

"Timu yetu imekuwa ikifanya vizuri katika mashindano hayo ambayo yanaandaliwa na klabu ya kuogelea ya Mwanza (MSC). Tulishinda mwaka 2016 na mwaka 2017 na 2018 tulimaliza katika nafasi ya pili. Mikakati yetu ni kuweka historia mwaka huu,” alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...