Na Chalila Kibuda, Michuzi TV
Chuo cha Mwalimu Nyerere Memorial Academy kimesema  licha ya kufundisha kozi mbalimbali pia wanafundisha maadili.

Akizungumza na waandishi wa habari Katika Maonesho ya Vyuo Vikuu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Mkuu wa Idara ya Elimu ya Juu wa Chuo hicho Dkt.Philip Daninga amesema kuwa  Wanafunzi katika maonesho hayo kwani wanadahili hapo hapo .

Amesema kuwa Wanafunzi wakisoma hapo wanajengwa kimaadili na kufanya kuweza kujitambua katika maisha yao. Dkt.Daninga amesema wanakozi mbalimbali katika Chuo hicho ambapo vijana wanaweza kusoma kutokana na kuwa Mazingira rafiki ya kusoma.

Aidha amesema kuwa maonesho hayo ni fursa ya kuwafikia wanafunzi ikiwa kutoa taarifa mbalimbali za Chuo hicho. "Tumedhamiria kutoa elimu bora inayokwenda na Mazingira ikiwa ni pamoja kuwafanya vijana kuwa wabunifu"amesema Daninga.
 Mwanafunzi wa Chuo cha Mwalimu Nyerere Memorial Academy Jenipher Siriwa akitoa ubunifu wake wa Umeme wa Jua  katika mfumo wa kufuata Jua Katika Maonesho ya Vyuo Vikuu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Mwanafunzi wa Chuo cha Mwalimu Nyerere Memorial Academy Mohamed Abushiri  akitoa maelezo namna alivyogundua kuzuia gesi kulipuka katika maonesho ya Vyuo Vikuu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Idara ya Elimu ya Juu wa Chuo cha Mwalimu Nyerere Memorial Academy Philip Daninga akizungumza na waandishi habari katika Maonesho ya Vyuo Vikuu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...