NA MWAMVUA MWINYI,PWANI

MWAJUMA Omary Malembeka (28)anadaiwa kumuua mume wake Selemani Kondo (43) mkulima na mkazi wa Chamalale,kata ya Vihingo,Mzenga ,wilayani Kisarawe mkoani Pwani, kwa kumchoma na bisibisi kwenye bega .

Akithibitisha kuhusu tukio hilo,kamanda wa polisi mkoani hapo, Wankyo Nyigesa alisema mwanamke huyo alifanya maamuzi hayo kutokana na wivu wa kimapenzi.

Alieleza, kulikuwa na mzozo baina yao ambapo Mwajuma alimtuhumu mume wake kuwa siyo mwaminifu katika ndoa yao."Selemani aliuawa kwa kuchomwa bisibisi katika bega lake la kushoto na sehemu ya juu na mke wake huyo"alifafanua.

Wankyo alisema, kujichukulia sheria mkononi sio jambo la msingi kwani inaweza kuleta madhara kama ya kujeruhi ama kusababisha kifo ,na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo zinazomkabili.

Katika hatua nyingine, huko kijiji cha Lulenga, Ubena ,jimbo la Chalinze polisi walimkamata Kitenye Lumange ,mfugaji wa jamii ya kimasai (24) kwa kosa la wizi wa ng'ombe 13 wenye thamani ya sh.milioni 7.2 mali ya Arisen Hussein mkazi wa kijiji cha Visakazi .

Kamanda huyo alibainisha,wanawasaka watuhumiwa wengine walioshiriki kuiba mifugo hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...