Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (aliyenyoosha mikono), akizungumza wakati alipotembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwenye maonesho ya nanenane kwenye viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu. Maonesho hayo yaliyobeba kaulimbiu ya "Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ukuaji wa Uchumi wa nchi yamefunguliwa rasmi Agosti 1, 2019 na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na yatafikia kilele Agosti 8, 2019.
Mhe. Bashe (kulia), akisindikizwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Elisante Ole Gabriel (kushoto) na Meneja wa Idara ya Uhusioano wa Umma na Itifaki, (BoT), Bi. Zalia Mbeo (katikati), wakayti akitoka kwenye banda hilo baada ya kulitembeekla.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe, (kulia), akisainin kitabu cha wageni huku akisikilizwa na Afisa Uhusiano Mkuu, Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki wa BoT Bw. Lwaga Mwambande (kushoto).
Mhe. Bashe akiuliza maswali ili kupata ufafanuzi kutoka kwa watumishi wa BoT alipotembelea banda la taasisi hiyo inayosimamia masuala ya kifedha hapa nchini. (Picha:Innocent Mmari-BoT).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...