Katibu wa UVCCM mkoa wa Katavi Theonas Kinyonto akizungumza na waandishi wa habari


Na Mwandishi wetu, Katavi

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Katavi umempongeza Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa utekelezaji wa miradi mikubwa mkoani Katavi

Akitoa pongezi hizo Katibu wa UVCCM mkoa bwana Theonas Kinyonto amesema ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mpanda hadi Tabora unaashiria utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho ya mwaka 2015/20

Aidha kupitia mradi wa uboreshaji miji utekelezaji wa mradi wa barabara ya lami ya kilometa 7.7 katika manispaa ya Mpanda uliogharimu shilingi bilioni 8 ambao kwa sasa umekamilika kwa asilimi 97

Pia wamemsukuru Rais kwa kutoa fedha za kujenga kituo kikubwa cha mabasi halikadhalika kuboresha miundombinu ya afya katika mkoa wa Katavi sanjari na ujenzi wa Hospitali za Wilaya tatu katika mkoa wa Katavi

Katika hatua nyingine bwana Kinyonto ametoa wito kwa Vijana kujiunga katika makundi ili kupata mikopo ya Halamshauri ambapo jumla ya shilingi milioni 700 zimetengwa kwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya kuwezesha makundi mbalimbali

Pia amepongeza suala la kutolewa kwa elimu bure jambo ambalo limeongeza uandikishaji wa wanafunzi mashuleni ambapo pia amewashukuru wazazi kwa kujitolea nguvu zao katika kufanikisha ujenzi wa vyumba vya madarasa

Aidha amewakumbusha vijana kuwa kupitia miradi yote inayotekelezwa na serikali ni fursa za ajira kwa vijana hivyo hawana budi kuzitumia fursa hizo vizuri

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...