Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Everist Ndikilo akizungumza wakati wa kikao chake na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (kushoto) kuzungumzia udhamini wa Benki hiyo kwenye Maonyesho ya Wiki ya Viwanda mkoa wa Pwani 2019 yatakayofanyika kati ya Oktoba 29 hadi Novemba 4, 2019, Kibaha Mkoani Pwani. Benki ya CRDB imedhamini maonyesho hayo kwa kutoa kiasi cha Milioni 60.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati) akifafanua jambo wakati wa kikao na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Everist Ndikilo (kulia) wakati wa kuzungumzia udhamini wa Benki hiyo kwenye Maonyesho ya Wiki ya Viwanda mkoa wa Pwani 2019 yatakayofanyika kati ya Oktoba 29 hadi Novemba 4, 2019, Kibaha Mkoani Pwani. Benki ya CRDB imedhamini maonyesho hayo kwa kutoa kiasi cha Milioni 60. Kushoto ni Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Bi. Theresia Mmbando (aliyesimama) akizungumza jambo wakati akitoa utambulisho kwa ugeni aliofatana nao.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...