IDADI kubwa ya watalii kutoka nchini Dernmark wamekuja wamefunga safari kwenda katika Kata ya Kata ya Magata mkoani Kagera kwa ajili ya kuona vivutio vya utaliii vilivyopo kwenye Kata hiyo.

Inaelezwa kuongezeka kwa idadi ya watalii kwenye Kata hiyo kutokana na mazingira mzuri ya uwepo wa huduma mbalimbali za kijamii pamoja na kuwa na maeneo mengi ya Utalii.

Akizungumza na Michuzi Blog Mkurugenzi wa Bukoba Tours William Rutta amesema kuwa katika hiyo kuna vitu vingi ambavyo vinapendwa na watalii na kuongeza wakazi wa eneo hilo ni wakarimu na wakulima wazuri wa Vanilla.

"Pamoja na kutembelea maeneo ya Utalii,watalii wengi wamefurahi uwepo wa huduma za kijamii,"amesema na kuongeza kuwa hifadhi ya mpya ya Burigi iliyopo Chato nayo itakuwa chachu ya kuongeza watalii katika Kata hiyo na Mkoa wa Kagera.

Rutta ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Ishozi iliyopo mkoani Kagera amesisitiza watalii wake watakuwa wakiweka kambi kata ya Magata wanapokuwa wanaendaa Hifadhi mpya ya Burigi Chato na Rubondo.

Pia ametoa shukrani kwa mwenyeji wake ambaye ni Katibu Mwenezi ww CCM Kata ya Magata Mansoor Amr kwani amekuwa akishiriki hatua kwa hatua kuhakikisha watalii wanapokelewa vizuri.

Kuhusu watalii hao amesema wametoka nchini Dernmak na kuongeza wamefurahishwa na ukarimu wa Watanzania huku wakieleza namna ambavyo wanaguswa na Rais John Magufuli kwa jinsi anavyowatumikia wananchi pamoja na kutangaza vema Tanzania.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...