CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR KINAPENDA KUUTANGAZIA UMMA NA WOTE WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA CHUO KWA MWAKA WA MASOMO 2019/2020 KWA NGAZI YA CHETI, STASHAHADA NA SHAHADA YA KWANZA KUWA, ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KATIKA AWAMU ZOTE.

INAPATIKANA KATIKA TOVUTI YA CHUO www.suza.ac.tz.
IKIWA KUNA MWANAFUNZI AMECHAGULIWA NA KWA BAHATI MBAYA JINA LAKE HALIKUTOKEA KATIKA ORODHA HII, ANAOMBWA AFIKE KATIKA KAMPASI YOYOTE YA CHUO ILIYO KARIBU NAE, AU AWASILIANE

 NA MAAFISA HUSIKA KWA UTATUZI WA HARAKA.
AIDHA, CHUO KINAPENDA KUUJUULISHA UMMA KUWA, TAREHE 4/11/2019 NDIO TAREHE RASMI YA KURIPOTI CHUO.

 WANAFUNZI WOTE WALIOCHAGULIWA WANAOMBWA KUWASILI CHUONI KATIKA KAMPASI KUU (TUNGUU) SAA MBILI KAMILI ZA ASUBUHI KATIKA UKUMBI WA DR. ALI MOHAMED SHEIN.

SAMBAMBA NA HILO, ZOEZI LA UPIMAJI WA AFYA KWA WANAFUNZI WOTE WALIOCHAGULIWA AMBALO LIMEANZA TAREHE 28/10/2019 LINAENDELEA HADI TAREHE 8/11/2019 MUDA WA SAA ZA KAZI.

TANBIH
WANAFUNZI WOTE WALIOCHAGULIWA WANASHAURIWA KUJA NA NYARAKA ZOTE WALIZOTUMIWA KATIKA AKAUNTI ZAO ZA UDAHILI KWA UFAFANUZI ZAIDI ILI KUONDOWA USUMBUFU USIO WA LAZIMA.

KARIBUNI SANA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...