Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Profesa Adolf Mkenda akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Makatibu wakuu na Watendaji Wakuu katika Mkutano unaoendelea Katika Kituo cha Kimataifa cha mikutano AICC Jijini Arusha.
Domingos Gove Mkurugenzi Mkuu wa Idaravya Chakula na Kilimo na Maliasili kwenye Sekretatieti ya SADC
Makatibu wakuu na Watendaji wakuu kutoka nchi za SADC wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mkutano huo kufunguliwa rasmi.
Mkutano ukiendelea katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano AICC Jijini Arusha.


Na.Vero Ignatus,Arusha.

Mkutano wa Makatibu wakuu na watendaji wakuu wa nchi wanachama wa jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika SADC Unaohusu masuala ya Mazingira Maliasili na Utalii umeanza leo Jijini Arusha

Aidha Mkutano huo ukiwa na lengo la kujadili mabadiliko ya tabianchi kwa nchi wananchama ambapo watapokea pia taarifa mbalimbali kuhusiana na kukabiliana Ujangili unaovuka mipaka ,kuwalinda wanayama pori na misitu.

Katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii Profesa Adolfu Mkenda alisema kuwa kwa sasa upo mjadala mkubwa ambao unaendelea kama utekelezaji wa itifaki mbalimbali za jumuiya hiyo ikiwemo ya vizuizi itifaki ya maeneo ikiwemo pia viendelee kuwepo na vizuizi vingine vipya vilivyowekwa kama vinafaa kwa maendeleo ya nchi hizo za SADC

Katibu Mkuu wa Wizara ,Profesa Adolfu Mkenda akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa makatibu wakuu kutoka nchi mwanachama amesema kuwa mkutano huo utajadili mambo mbalimbali ikiwemo vita dhidi ya ujangili ambayo inapaswa kuungwa mkono kwa nchi zote mwanachama badala kuachwa kwa nchi moja.

“Ifahamike kuwa Tanzania ni miongoni mwa wananchama wa SADC wanaotekeleza mkakati kuhusu usimamizi wa sheria na vita dhidi ya ujangili wa wanayamapori na maeneo mengine yanayohusu mipango ya uhifadhi yaliovuka mipaka wan chi moja kwenda nyingine kwenye maeneo ya misitu uvuvi mazingira na mabadiliko ya tabianchi”alisema Prof.Mkenda

Mkenda amesema kuwa nchi moja ni vigumu kupambana na ujangili hivyo tunahitaji kuunganisha nguvu kwa nchi zote ili ziweze kufanikisha juhudi za kupambana na ujangili.“Tunahitaji kuwa na mpango mkakati wa kukuza utalii katika nchi za SADC hii ni moja kati ya agenda muhimu zitakazojadiliwa” Alisema Profesa Mkenda

Mkurugenzi wa idara ya Chakula ,kilimo na Maliasili kutoka Sektretarieti ya SADC ,Domingos Zephania Gove amesema kuwa wanahitaji kutembea pamoja kama nchi za SADC katika kuweka mikakati katika masuala ya kimazingira,Utalii na Wanyamapori 

Gove amesema kuwa wanahitaji kuthibitisha program za pamoja za kukuza utalii na kusimamia maliasili katika ukanda husika.

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Raisi ,Muungano na Mazingira ,Mhandisi Joseph Malongo amesema kuwa watajadili mkakati wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi kwa pamoja na jinsi ambavyo wananchi wanaweza kutumia uchumi wa bluu kwa maana ya bahari katika kuchangia maendeleo .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...