Na Chalila Kibuda, Michuzi TV
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema kuwa Msanii wa Vichekesho Idriss Sultan hajalipoti katika kituo chochote cha Polisi kufuatia na Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam la kumtaka msanii huyo kujisalimisha katika kituo cha Polisi kwa kutumia picha yenye nembo ya alama ya taifa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania.
Akizungumza na Michuzi TV Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Razaro Mambosasa amesema kuwa Msanii huyo anatafutwa na hakuna taarifa ya kuripoti katika kituo cha Polisi chochote cha jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa Msanii Idriss Sultan anatafutwa na Jeshi la Polisi na mara baada kuripoti au kukamatwa lazima ahojiwe kwa kile alichokifanya kwa kutumia alama za Taifa kutumia bila mamlaka.
Msanii Idriss Sultan alipiga picha na kuweka nembo ya Kiti anachotumia Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania wakati ikiwa ni siku ya kuzaliwa kwa Rais Dkt.John Pombe Magufuli Oktoba 29.
Baada ya picha Idriss Sultan kusambaa katika mitandao ya Jamii Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda aliandika katika mtandao wake kwa kumtaka Msanii huyo afike katika kituo chochote cha Polisi na kusema kuwa taarifa atazikuta huko.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema kuwa Msanii wa Vichekesho Idriss Sultan hajalipoti katika kituo chochote cha Polisi kufuatia na Agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam la kumtaka msanii huyo kujisalimisha katika kituo cha Polisi kwa kutumia picha yenye nembo ya alama ya taifa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania.
Akizungumza na Michuzi TV Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Razaro Mambosasa amesema kuwa Msanii huyo anatafutwa na hakuna taarifa ya kuripoti katika kituo cha Polisi chochote cha jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa Msanii Idriss Sultan anatafutwa na Jeshi la Polisi na mara baada kuripoti au kukamatwa lazima ahojiwe kwa kile alichokifanya kwa kutumia alama za Taifa kutumia bila mamlaka.
Msanii Idriss Sultan alipiga picha na kuweka nembo ya Kiti anachotumia Rais wa Jamhuri ya Muungano Watanzania wakati ikiwa ni siku ya kuzaliwa kwa Rais Dkt.John Pombe Magufuli Oktoba 29.
Baada ya picha Idriss Sultan kusambaa katika mitandao ya Jamii Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda aliandika katika mtandao wake kwa kumtaka Msanii huyo afike katika kituo chochote cha Polisi na kusema kuwa taarifa atazikuta huko.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...