Na Mwandishi wetu, Kibaha
Serikali imepongeza uwekezaji unaofanywa na Benki ya Maendeleo ya TIB kwa kuwezesha uwekezaji kwa viwanda na makampuni ya wazawa hivyo kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje ya nchi.
Pongezi hizo zilitolewa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stella Manyanya wakati alipotembelea Banda la Benki ya Maendeleo TIB wakati wa Maonesho ya Wiki ya Viwanda ya Mkoa wa Pwani yanayoendelea mjini Kibaha.
Mhandisi Manyanya aliyekuwa akimwakilisha Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan katika uzinduzi wa maonesho hayo alisema kuwa uwekezaji unaofanywa na Benki ya Maendeleo TIB umechangia kwa kiasi kikubwa kuondoa utegemezi wa bidhaa kutoka nje ya nchi na kutoa ajira kwa Watanzania.
Kwa upande wake Naibu wa Waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu alitumia fursa hiyo kuwahakikishia wazalishaji wa nyaya na vifaa vya umeme kuwa waendelee kuzalisha vifaa bora, kwa kuwa soko la bidhaa hizo lipo hasa kwa kuzingatia uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika sekta ya nishati.
“Naomba niwahakikishie kuwa soko la bidhaa zenu lipo na kama mnavyofahamu Serikali imezuia uingizaji wa bidhaa kutoka nje ambazo zinaweza kuzalishwa na wawekezaji wa ndani ya nchi,” alisema.
Akizungumza wakati wa kumkaribisha Mgeni Rasmi, Mkurugenzi wa Mipango na Mikakati wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Patrick Mongella alisema kuwa TIB ikiwa benki ya kisera inatekeleza kwa vitendo juhudi za serikali kwa kuwezesha uwekezaji wa viwanda nchini ili kuongeza ajira na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje.

“Benki ya Maendeleo TIB ni taasisi ya kifedha ambayo imekuwa ikisaidia nchi katika ukuaji wa uchumi na maendeleo katika sekta za kimkakati, hivyo tunatekeleza mikakati ya Serikali inayolenga kuchagiza maendeleo ya haraka ya kiuchumi,” alisema.
Mkurugenzi wa Mipango na Mikakati wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Patrick Mongella (wapili kulia) akitoa maelezo kwa Mgeni Rasmi wa Ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya Viwanda ya Mkoa wa Pwani, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stella Manyanya (watatu kushoto). Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo (wapili kushoto).
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stella Manyanya (watatu kushoto) akiwa na Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo (wapili kushoto) wakiangalia nyaya za umeme zinazozalishwa na Kampuni ya Konnectt Wire moja ya wateja waliowezehswa na Benki ya Maendeleo TIB.
Mkurugenzi wa Mipango na Mikakati wa Benki ya Maendeleo TIB, Bw. Patrick Mongella akimkabidhi zawadi Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...