Shirika
 la Reli Tanzania – TRC pamoja na ‘Clouds Media Group’ (CMG) 
wameadhimisha miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage 
Nyerere kwa kufanya safari ya kihistoria kutoka Dar es Salaam kuelekea 
Dodoma kwa kutumia treni ya Deluxe kwa lengo la kuenzi mawazo ya Baba wa
 taifa ya kuhamasisha watanzania kuhamia makao makuu ya nchi jijini 
Dodoma kwa kutumia usafiri wa treni hivi karibuni, Oktoba 2019.
Katika
 safari hiyo Menejimenti ya Shirika la Reli Tanzania ikiongozwa na 
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Ndugu Masanja Kungu 
Kadogosa  iliungana na timu kutoka ‘Cloud Media Group’, timu ya Tigo 
Fiesta pamoja na wasanii zaidi ya 200 kuelekea Dodoma kuadhimisha miaka 
20 ya Baba wa Taifa lakini pia kutoa burudani na hamasa kwa  wananchi wa
 mkoa wa Dodoma.
Licha
 ya kujionea Vivutio kibao vya nchi yetu ikiwemo maajabu ya mto Ruvu 
kwenye Safari ya kihistoria kati ya CMG na TRC, timu ya Tigo Fiesta 2019
 imefanikiwa kujionea utendaji kazi wa wakandarasi waliopewa dhamana na 
Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli 
kujenga Reli ya Kisasa – SGR kuanzia Dar e Salaam hadi Makutupora mkoani
 Singida ambapo wasanii walitembelea Kilosa katika eneo ambalo handaki 
refu zaidi nchini linajengwa.
Katika
 safari hii ya kuadhimisha miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. 
Julius K. Nyerere, TRC na  CMG walihakikisha uwepo wa Mwl. Nyerere ndani
 ya treni ambapo vitu kadhaa ambavyo vilipendwa na Baba wa Taifa 
vilienziwa ikiwemo mchezo wa Bao ambao alikuwa akiupenda, hotuba zake 
pamoja na vyakula pendwa vya Mwl. Nyerere navyo vilipikwa katika safari 
hiyo. 
Aidha
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli alionekana akifurahia mchezo wa Bao 
na baadhi ya wafanyakazi wa CMG, naye ACP S.K Kulyamo, Kamanda wa Jeshi 
la Polisi Kikosi cha Reli pia ni moja kati ya watu ambao siku ya leo 
alikuwa kwenye safari ya treni kutoka Dar mpaka Dodoma kuhakikisha 
usalama wa wasafiri, kubwa ni kuweza kuandika historia kwa kumuenzi Baba
 wa taifa na kuweza kukumbuka kifo cha Baba wa Taifa ndani ya treni 
ikiwa ni miaka 20 toka atangulie mbele za haki.
Naibu
 Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira 
Mhe. Anthony Mavunde amelipongeza Shirika la Reli Tanzania kwa mapinduzi
 makubwa yaliyofanyika katika kipindi kifupi pia amefurahi kuona wasanii
 wengi wameingia Dodoma kwa kutumia usafiri wa treni na anaamini kwamba 
wasanii wamefurahi, wamejifunza mengi na watakuwa mabalozi wazuri kuhusu
 usafiri wa reli pamoja na Mradi mkubwa wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa.
Mkurugenzi
 Mkuu wa TRC Ndugu Masanja Kungu Kadogosa kwa niaba ya Shirika 
amemshukuru Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kudumisha mawazo ya 
Mwalimu kwa kuhamisha serikali mjini Dodoma na kuboresha miundombinu ya 
reli ambayo ndio msingi mkuu wa usafirishaji nchini, pia amewashukuru 
Naibu Waziri Mhe. Anthony Mavunde, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. 
Patrobas Katambi, timu ya CMG na wasanii kwa ujumla katika maadhimisho 
ya miaka 20 ya Baba wa Taifa na amesema kuwa ana imani kwamba safari 
hiyo iimesaidia kutunza historia kuhusu maisha ya Baba wa taifa. 



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...