***********************************

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amezindua chumba cha kuhifadhia majokofu yanayotumia umeme wa jua kwenye zahanati ya Nyakasungwa iliyopo halmashauli ya Buchosa wilayani Sengerema.

Halmashauri ya buchosa imepata majokofu 17 kutoka Wizara ya afya mwezi oktoba 2019 kwa awamu ya kwanza na tayari yamesambazwa kwenye na kufungwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Hali ya chanjo kwa halmashauri hiyo kwa kwa mwaka huu ni asilimia 94 kutoka asilimia 79 mwaka jana na katika kampeni ya kitaifa ya chanjo ya surua na rubella mwezi oktoba mwaka huu imefanikiwa kwa asilimia 106.

Majokofu hayo yatasaidia kuimarisha mnyororo baridi na hivuo kuongeza ubora na utunzaji wa chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya ambayo itapelekea watoto kupata chanjo zenye ubora kama ilivyokusudiwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...