Maafisa waandamizi 21 wa Jeshi la nchi ya Bangladesh hivi karibuni wametembelea Tanzania kujionea vivutio mbalimbali vya kitalii ikiwa ni pamoja na Ngorongoro na Zanzibar.
Maafisa hao, kutoka Chuo cha kijeshi kiitwacho Bangladesh Defence services Command and Staff College cha mjini Dhaka walipata hamasa ya kutembelea Tanzania baada ya mwanafunzi mwenzao na afisa wa JWTZ Meja Rajabu Mangapi aliye mafunzoni chuoni hapo kufanya presentantion iliyohusu utalii, viwanda, miundombinu na mikakati ya kuipeleka Tanzania katika uchumi wa viwanda.
Presentantion hiyo ilihudhuriwa pia na wafanyabiashara wakubwa ambao pia walihamasika vilivyo na kuonesha nia kuja kuwekeza Tanzania kwa kujenga viwandani.
Watalii hao wamemwambia ripota wetu aliyeko Ngorongoro kwamba hawakuweza kuamini macho yao kuona wanyama wa aina zote wakiishi bega kwa bega na wanadamu huko 'Shimoni' Ngorongoro, na kuuliza endapo kama eneo hilo sipo ilipotua Safina ya Nuhu baada ya dhoruba?
Walimshukuru sana Meja Mangapi ambaye presentation yake ya kuvutia iliwafanya wafikie uamuzi wa kuja kujionea wenyewe, na kukuta kumbe walichooneshwa na mwanafunzi mwenzao huy pale chuoni kumbe ni theluthi tu ya maajabu ya Tanzania.
Watalii hao wamemwambia ripota wetu aliyeko Ngorongoro kwamba hawakuweza kuamini macho yao kuona wanyama wa aina zote wakiishi bega kwa bega na wanadamu huko 'Shimoni' Ngorongoro, na kuuliza endapo kama eneo hilo sipo ilipotua Safina ya Nuhu baada ya dhoruba?
Walimshukuru sana Meja Mangapi ambaye presentation yake ya kuvutia iliwafanya wafikie uamuzi wa kuja kujionea wenyewe, na kukuta kumbe walichooneshwa na mwanafunzi mwenzao huy pale chuoni kumbe ni theluthi tu ya maajabu ya Tanzania.
![]() |
Maafisa kutoka Chuo cha kijeshi cha Bangladesh Defence services Command and Staff College wakitembelea Ngome Kongwe huko Zanzibar wakati wa kutalii Tanzania |
![]() |
Maafisa kutoka Chuo cha kijeshi cha Bangladesh Defence services Command and Staff College wakitembelea Bwawa la Viboko huko Ngorongoro wakati wa ziara yao ya kitalii nchini Tanzania |
![]() |
Maafisa kutoka Chuo cha kijeshi cha Bangladesh Defence services Command and Staff College wakijitayarisha kuingia 'shimoni' Ngorongoro wakati wa ziara yao ya kitalii nchini Tanzania |
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...